Connect with us

News

Murkomen: Polisi kupokea nyongeza ya mshahara

Published

on

Waziri wa usalama wa ndani Kipchumba Murkomen amesema serikali inalenga kufanikisha nyongeza ya mishahara ya maafisa wa polisi kote nchini kwa asilimia 10. 

Waziri Murkomen alisema mpango huo utatekelezwa kwa awamu na kwa kuambatana na bajeti ya serikali ya mwaka wa kifedha wa 2025/2026 ili kuwapa motisha maafisa wa polisi na kufanikisha utendakazi bora.

Akizungumza katika kaunti ya Nandi wakati wa kikao cha baraza la usalama maarufu Jukwaa la usalama, Waziri Murkomen aliwataka maafisa wa polisi kuwa na subra wakati suala hilo linaposhughulikiwa.

“Serikali iko na mpango maalum wa kuhakikisha maaskari wetu wanapokea nyongeza ya mishahara kwa asilimia 10 na hii ni kuhakikisha tunawapa motisha maafisa wetu wa usalama na nitekelezwa kupitia Ofisi ya huduma ya polisi nchini na ile ya Inspekta jenerali wa polisi”, alisema Murkomen.

Waziri Murkomen alidokeza kwamba tatizo la majangili katika maeneo ya Pokot Magharibi, Turkana, Samburu, Baringo, na Elgeyo Markwet kama changamoto kuu ya kiuslama katika maeneo ya Bonde la Ufa, akisema serikali inafuatilia kati ya bunduki haramu elfu 5 hadi elfu 10 zinazomilikiwa na majangali.

“Tuko na tatizo kubwa katika maeneo ya bonde la Ufa hasa Pokot Magharibi na kule Baringo na Samburu lakini tumejipanga kama idara ya usalama tutahakikisha kumesambaratisha hao majangili na kurudisha bundiki zote haramu ambazo wanatumia kuhangaisha watu”, alieleza Murkomen.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending