News
Mwili wa marehemu Samuel Kirao wafukuliwa
Hatimaye familia ya Marehemu Samuel Kirao Charo imepata haki ya kuuzika mwili wa mpendwa wao baada ya mzozo uliokuwepo hapo awali na kupelekea marehemu kuzikwa kwa mujibu wa dini ya Kiislamu.
Hii ni baada ya familia hiyo kushinda kesi kwenye Mahakama ya Malindi wakati ambapo Mahakama ya Kadhi ilikuwa imeidhinisha jamii ya Waislamu kuuzika mwili huo kwa msingi kwamba Marehemu alikuwa muislam hata wakati wa kufa kwake.
Jaji Mugure Thande wa Mahakama ya Malindi alitoa uamuzi wa kufukuliwa kwa mwili huo na kisha ukabidhiwe familia yake ili uzikwe upya baada ya familia kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa Mahakama ya Kadhi.
Eunice Kirao ambaye ni mama mzazi wa marehemu alisema marehemu alisilimishwa akiwa na akili punguani, akieleza kusikitishwa na jamii hiyo ya waislamu kutowapatia nafasi na badala yake ikashurutisha ibada ya mazishi kwa nguvu.
Kwa upande wake babake marehemu Stephen Kirao alisema wamepitia gharama nyingi za kuandaa mazishi kabla ya jamii ya waislamu kuuzika mwili wa marehemu, akisisitiza kuwa ni sharti gharama hizo zilipwe.

Familia ya Marehemu Samuel Kirao Charo katika makaburi ya Takaungu
Naye Kalume Charo ambaye ni kakake mkubwa marehemu alieleza kwamba hali haijakuwa nzuri muda wote huo kwani wamekuwa wakipitia kejeli na unyanyapaa katika eneo wanaloishi mbali na wazazi wao kuathirika kiafya.
Ikumbukwe kwamba marehemu Samuel aliuawa na umma baada ya kumuua kwa kumdunga kisu Ustadh mmoja eneo la Takaungu na kisha kuula utumbo wake.
Taarifa ya Hamis Kombe
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

