Connect with us

News

Mwashako, amtaka Waziri Duale kuwataja wanaohusika na sakata ya SHA

Published

on

Mbunge wa Wundanyi Danson Mwashako alielezea kukerwa na madai ya ufisadi yanayoendelea kushughudiwa humu nchini hasa kwenye Bima ya afya ya jamii nchini SHA.

Mwashako alisema ni jambo la kusikitisha kuona viongozi wakijadili suala hilo bila kuchukua hatua zozote mwafaka, hali ambayo inachangia wananchi wengi kutokuwa na imani na viongozi wao.

Mwashako ambaye pia ni Mwenyekiti wa Muungano wa wabunge wa Pwani alimtaka Waziri wa Afya nchini Aden Duale kuwataja hadharani wale wanaohusika na sakata za ufisadi kwenye bima hiyo, akisisitiza kwamba hatua hiyo itasaidia kuimarisha utendakazi wake kama Waziri.

“Kila siku pesa zinapotea, tuseme tu ukweli mimi kama Mwashako inanisumbua sana ndio maana  nasema sisi kama viongozi hata mbinguni hatutaenda na siku zote nimekuwa nikimwambia Duale kama uchunguzi imefanywa basi asiogope awataje hadharini wale wetu walihusika na kuiba pesa ya SHA kwa sababu ukiangalia E-Citizen pesa pia inaibwa kila siku”, alisema Mwashako.

Wakati huo huo, alivilaumu vitengo vya usalama nchini hasa Idara ya ujasusi nchini NIS na Idara ya upelelezi wa jinai nchini DCI kwa kuzembea kuwajibikia majukumu yao huku wananchi wakikabiliwa na madhara kutokana na hali hiyo.

Kauli yake ilijiri huku Kamati ya Afya katika bunge la kitaifa ikiongozwa na Mwenyekiti wake ambaye pia ni mbunge wa Seme Dkt James Nyikal ikiilaumu Wizara ya Afya nchini kwa kuharibu utekelezaji wa uzidunzi wa Mamlaka ya Afya ya jamiI SHA.

Viongozi wa kamati hiyo walisema changamoto hizo zinaathiri huduma za hospitali mbalimbali za umma nchini sawa na kuwakosesha wagonjwa wengi huduma muhimu za afya.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending