Connect with us

News

Mzee wa miaka 69 ahukumiwa miaka 25 jela kwa kumnajisi mjukuu wake wa miaka 13

Published

on

Mahakama ya Kilifi imemhukumu kifungo cha miaka 25 gerezani mwanaume mmoja ambaye ni mzee wa umri wa miaka 69 baada ya kupatikana na hatia ya kumnajisi mjukuu wake mwenye umri wa miaka 13.

Akitoa hukumu hiyo, Hakimu Ivy Wasike amesema mzee huyo atatumikia kifungo hicho gerezani kwani wazee kama wao ndio wanaofaa kukemea vitendo hivyo sawa na kuelekeza vijana lakini wamekuwa wahusika wakuu wa dhulma za kijinsia dhidi ya watoto.

Hakimu Wasike ameagiza idara ya watoto na jamii kumpa ushauri nasaha mtoto huyo ili apate nafuu baada ya kutatizika kisaikolojia alipopitia dhulma hiyo.

Awali Mahakama ilielezwa kwamba kati ya tarehe tofauti mwezi Januari mwaka 2025 katika eneo la Kauma kaunti ya Kilifi, mzee huyo kwa jina Chivatsi Mundu akiwa mlevi alimnajisi mjukuu wake aliyekuwa ameenda kumsaidia kuchota maji.

Mahakama imeelezwa kwamba baada ya mzee huyo kumtendea unyama huo mjukuu wake alionya kwamba asiwahi kusimulia kitendo hicho kwa mtu yeyote tukio hilo, lakini ikabainika wazi.

Mahakama pia ikimpa mzee huyo siku 14 za kukata rufaa iwapo hajaridhishwa na uamuzi huo wa Mahakama.

Taarifa ya Teclar Yeri

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending