Connect with us

News

Vijiji vingi vimeathirika na mafuriko Tanariver

Published

on

Idadi kubwa ya familia zilizokuwa zikiishi karibu na Mto Tana katika kaunti ya Tana river zimeanza kuhama ili kutafuta maeneo salama ya kuishi kufuatia athari za mafuriko.

Familia hizo zimesema tayari mto huo umeanza kuvunja kingo zake kutokana na mvua kubwa inayoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali nchini, na kuathiri familia hizo.

Familia hizo kutoka vijiji vya Ziwani na Bula Punde katika eneo bunge la Garissa mjini, zimesema hazina mahali pa kuishi na watoto wao licha ya kuitikia wito wa Serikali na Idara ya utabiri wa hali ya hewa kuhamia maeneo salama.

“Tumeambiwa tuhame tuenda maeneo mengine salama kuepuka majanga lakini hatuna mahali pa kuenda, tumeondoka kweli katika makaazi yetu kwa sababu kumejaa marufiko baada ya Mto Tana kuvunja kingo zake hata hatuna mahali pakuishi watoto wananyeshwe, serikali ingetusaidia”, alisema mkaazi.

Athari za mafuriko katika vijiji vya kaunti ya Tanariver

Kwa upande wake, Gavana wa Tanariver Dhadho Godhana alisema japo serikali ya kaunti hiyo haijapokea idadi kamili ya walioathirika, juhudi zaidi zinaendelezwa kuhakikisha waathiriwa wanapata msaada huku akiwahimiza kuhamia maeneo salama.

“Tunashirikiana na baraza la magavana kuangalia vile tutasaidia watu wetu kupata msaada wa chakula na hata mavazi kwa sasa vijiji vingi vimeharibiwa na mafuriko lakini tunafatilia ili tujue ni watu wangapi wameathirika”,alisema Godhana.

Hata hivyo Kamishna wa kaunti hiyo Joseph Mwangi aliwarai wakaazi walio katika athari ya kuathirika na mafuriko kuchukua tahadhari na kuhamia maeneo salama, akisema serikali inalishuhulikia suala hilo.

Hata hivyo familia zilizoathirika zimeiomba serikali kuwasaidia na chakula cha msaada kwani sasa hali imekuwa ngumu kwao huku wakipendekeza serikali kuchimba mabwawa ili kuzuia mafuriko baada ya mto Tana kuvunja kingo zake.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wadau wa sekta ya uchukuzi wasitisha mgomo wao

Published

on

By

Maafisa wa sekta ya uchukuzi wameahirisha mgomo wao baada ya mazungumzo yaliyoongozwa na Rais William Ruto katika ikulu ya Mombasa.

Maafisa hao wakiongozwa na rais wa Muungano wa wamiliki wa matatu Albert Karagacha wamesema kuwa mengi ya masuala waliokuwa nayo ikiwemo kupanda kwa bei ya mafuta nchini yameangaziwa kwa kina na rais Ruto.

Karagacha amewataka wahudumu wa sekta ya uchukuzi wa umma pamoja na wamiliki wa magari ya uchukuzi wa mizigo kuhakikisha wanarudisha magari yao barabarani, akisema masuala waliowasilisha kwa rais yameangaziwa

Akizungumza mda mfupi baada ya kufanya kikao na rais William Ruto mjini Mombasa, Karagacha amesema serikali imekuwa kiangazia kwa kina masuala mbali mbali yanayohusu sekta ya uchukuzi nchini.

Aidha amesema iwapo bado serikali itakuwa inajikokota katika kufanikisha masuala waliojadiliana basi wataitisha mazungumzo zaidi na Wizara husika ili kuafikiwa kwa ajenda zao huku akisema japo suala la mzozo wa mafuta sio jambo la Kenya pekee lakini taifa inawajibu wa kusaidia wananchi wake.

Wakati huo huo Karagacha amewataka wakenya kutoingiza siasa katika suala la kupanda kwa bei ya mafuta nchini.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

News

Mshukiwa wa ulanguzi na usafirishaji wa watoto anyimwa dhamana

Published

on

By

Mahakama ya Shanzu imemnyima dhamana mshukiwa wa ulanguzi wa watoto zaidi ya 20.

Mahakama imeagiza mshukiwa huyo kuzuiliwa rumande ili kuwawezesha maafisa wa polisi kukamilisha uchunguzi wao.

Mahakama imeelezwa kwamba mshukiwa huyo Almasi Rama Amos mwenye umri wa miaka 27 alikamatwa na maafisa wa upelelezi kutoka kitengo cha kupambana na ulanguzi wa binadamu na ulinzi wa watoto (AHTCPU) pamoja na maafisa wa idara ya upelelezi wa Jinai kutoka kaunti ya Mombasa.

Kukamatwa kwake kufuatia wiki kadhaa za uchunguzi kuhusu ripoti za unyanyasaji wa watoto zinazowalenga wasichana wadogo walio katika mazingira magumu.

Rama, anayetuhumiwa kwa kujihusisha na kundi linalodaiwa kuwa la ulanguzi wa watoto na dhulma za kingono na kufikishwa katika Mahakama ya Shanzu kufuatia operesheni ya kiusalama iliyoidhinishwa na maafisa hao.

Rama alipatikana katika mtaa wa Nguu Tatu eneo la Concordia katika kaunti ndogo ya Kisauni akiwa na watoto watatu wa kike.

Mahakama imeelezwa kuwa mshukiwa anadaiwa kuendesha “vituo vya uokoaji” katika kaunti za Mombasa na Kilifi kwa kujifanya kuwalea na kuwapa ushauri.

Kulingana na uchunguzi vituo hivyo vilikuwa vikitumika kama msingi wa dhulma za kingono na unyanyasaji wa watoto.

Alipokamatwa, mshukiwa aliwaongoza maafisa hadi kituo chengeni eneo la Ribe katika eneo bunge la Rabai, ambapo maafisa wa upelelezi waliwaokoa watoto 19 wa jinsia ya kike na kufikisha jumla ya waathiriwa waliookolewa kufikia ishirini na wawili (22).

Mbele ya Mahakama ya Shanzu tarehe 21 Mei, 2026, mshukiwa amekabiliwa na mfululizo wa mashtaka, ikiwemo unajisi, biashara ya watoto kwa madhumuni ya kuwadhulumu kingono pamoja na unyanyasaji wa watoto ambapo amekana mashtaka hayo.

 Kesi hiyo imepangwa kutajwa Juni 8, 2026.

Taarifa ya Teclar Yeri

Continue Reading

Trending