Connect with us

News

Vijiji vingi vimeathirika na mafuriko Tanariver

Published

on

Idadi kubwa ya familia zilizokuwa zikiishi karibu na Mto Tana katika kaunti ya Tana river zimeanza kuhama ili kutafuta maeneo salama ya kuishi kufuatia athari za mafuriko.

Familia hizo zimesema tayari mto huo umeanza kuvunja kingo zake kutokana na mvua kubwa inayoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali nchini, na kuathiri familia hizo.

Familia hizo kutoka vijiji vya Ziwani na Bula Punde katika eneo bunge la Garissa mjini, zimesema hazina mahali pa kuishi na watoto wao licha ya kuitikia wito wa Serikali na Idara ya utabiri wa hali ya hewa kuhamia maeneo salama.

“Tumeambiwa tuhame tuenda maeneo mengine salama kuepuka majanga lakini hatuna mahali pa kuenda, tumeondoka kweli katika makaazi yetu kwa sababu kumejaa marufiko baada ya Mto Tana kuvunja kingo zake hata hatuna mahali pakuishi watoto wananyeshwe, serikali ingetusaidia”, alisema mkaazi.

Athari za mafuriko katika vijiji vya kaunti ya Tanariver

Kwa upande wake, Gavana wa Tanariver Dhadho Godhana alisema japo serikali ya kaunti hiyo haijapokea idadi kamili ya walioathirika, juhudi zaidi zinaendelezwa kuhakikisha waathiriwa wanapata msaada huku akiwahimiza kuhamia maeneo salama.

“Tunashirikiana na baraza la magavana kuangalia vile tutasaidia watu wetu kupata msaada wa chakula na hata mavazi kwa sasa vijiji vingi vimeharibiwa na mafuriko lakini tunafatilia ili tujue ni watu wangapi wameathirika”,alisema Godhana.

Hata hivyo Kamishna wa kaunti hiyo Joseph Mwangi aliwarai wakaazi walio katika athari ya kuathirika na mafuriko kuchukua tahadhari na kuhamia maeneo salama, akisema serikali inalishuhulikia suala hilo.

Hata hivyo familia zilizoathirika zimeiomba serikali kuwasaidia na chakula cha msaada kwani sasa hali imekuwa ngumu kwao huku wakipendekeza serikali kuchimba mabwawa ili kuzuia mafuriko baada ya mto Tana kuvunja kingo zake.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending