Connect with us

News

Naibu rais Prof. Kithure Kindiki amkosoa Uhuru Kenyatta

Published

on

Naibu wa rais Prof. Kithure Kindiki amemkosoa Rais mstaafu Uhuru Kenyata kutokana na matamshi yake dhidi ya serikali ya Kenya Kwanza.

Akirejelea suala aliloibua rais mstaafu Uhuru Kenyatta kuhusu mpango wa Linda Mama, Kindiki alisema mpango huo uliotekelezwa chini ya serikali ya Jubilee haukua wa kujumuisha wakenya wote.

Kindiki aliongeza kuwa bima mpya ya SHA inawafaidi wakenya wote bila ubaguzi.

Wakati huo huo Kindiki alimtaka rais huyo mstaafu kuikosoa serikali ya sasa kwa hekima badala ya lawama.

“Kuna watu wengi wanaleta mzaha kwa haya maneno ya afya ya umma, na wanaongea kiholela, na hawataki kusema hapo mbeleni hatukuwa na msingi dhabiti wa afya, sisi tunashukuru yale mambo rais William Ruto wakati alipokuwa naibu rais walianzisha na rais Uhuru Kenyatta mradi wa Linda Mama, sasa huu mradi mpya haumaanishi ya kwamba hatuka katika ule mpango wa kusaidi akina mama wajawazito kupitia Linda Mama”,alisema Kindiki.

Wakati huo huo viongozi wa kaunti ya Mombasa wakiongozwa na gavana Abdhulswamad Sharrif Nassir na mbunge wa Likoni Mishi Mboko, walishutumu viongozi wa upinzani wanaopinga miradi ya serikali, wakisema upinzani haujawakuwa na manufaa kwa mwananchi wa kawaida.

Viongozi hao walimkosoa moja kwa moja rais mstaafu Uhuru Kenyatta, wakidai kuwa anachochea siasa badala ya kutoa ushauri mwafaka kwa serikali iliyoko mamlakani.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending