Connect with us

News

Nyamu: Jamii ni lazima ielemishwe kuhusu haki zao

Published

on

Mwanasayansi na mkurugenzi mkuu wa shirika la kaungazia masuala ya Ndovu Jim Justus Nyamu pamoja na wanaharakati wa masuala ya wanyamapori wametoa wito kwa serikali pamoja na wadau husika kuhakikisha jamii zinaelimishwa kuhusu haki zao za namna ya kupata fidia kutokana na athari za wanyamapori.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari huko Mombasa, Nyamu alisema visa vya wanyamapori kuharibu mimea na hata kusababisha vifo na majeraha vimekuwa vikiendelea huku wananchi wengi wakikosa kufahamu taratibu za kufidiwa.

Nyamu pia alisema kunapaswa kuwa na hamasa za mara kwa mara, vijijini na maeneo ambayo yako karibu na hifadhi za wanyamapori ili wananchi wafahamu hatua ambazo wanapaswa kuchukua wanapopata hasara zinazosababishwa na wanyamapori.

Vilevile, Nyamu alitoa wito kwa serikali kuu kupitia wizara husika kuimarisha mfumo wa kulipa fidia kwa kuhakikisha unakuwa wa haraka, uwazi na haki kwa kila mmoja ambaye ameathiriwa na wanyamapori.

Naye Kamishna wa kaunti ya Mombasa Mohamed Noor alisema serikali iko tayari kushirikiana na mashirika mbalimbali ya kijamii ili kuwaelimisha Wakenya kuhusu haki zao na pia kuimarisha mfumo wa utoaji wa fidia kwao.

Taarifa ya Janet Shume

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending