News
Ogamba awaonya walimu wakuu dhidi ya kuwarudisha wanafunzi nyumbani
Waziri wa Elimu nchini Julius Migos Ogamba amewaonya Walimu wakuu dhidi ya kuwarudisha nyumbani wanafunzi ambao hawana karo ama sare za shule, akisema watakaopatikana watachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwemo kufutwa kazi.
Waziri Ogamba alisema sera ya serikali ya asilimia 100 ya wanafunzi kujiunga na shule inaendelezwa, akidoeza kwamba kufikia sasa ni asilimia 8 pekee ya wanafunzi ambao bado hawajajiunga na shule za Sekondari ya juu nchini.
Akizungumza na wadau wa sekta ya elimu jijini Nairobi, Ogamba aliwataka Walimu wakuu wa shule za Sekondari ya juu kuhakikisha wanatumia raslimali walizonazo shuleni ili kuhakikisha hakuna Mwanafunzi anakosa kujiunga na gredi ya 10.
“Tunashirikiana na waajiri wa walimu TSC, na Mwalimu wakuu watakaowarudisha wanafunzi wa gredi ya 10 nyumbani eti hawana karo ama sare za shule tutawachukulia hatua kwa sababu haina haja ya kurudisha wanafunzi wawili ama watatu kwa kukosa sare za shule, hiyo haitakubalika”,alisema Waziri
Wakati huo huo alidokeza kwamba tayari serikali imesambaza asilimia 50 ya fedha za kusimamia shughuli za masomo ya kalenda ya mwaka 2026, ili kuhakikisha shule hazikumbwi na changamoto.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

