News
Polisi wanachunguza mauaji ya mtoto wa miaka 7 Kilifi
Bwiwi la simanzi limeghubika wakaazi wa kijiji cha Kwa Nzai eneo la Mwezang’ombe kaunti ya Kilifi mapema leo baada ya msichana mwenye umri wa miaka 7 kupatikana amefariki baada ya kudaiwa kunajisiwa.
Wakaazi wa kijiji hicho wamekongama katika eneo la tukio kushuhudia maafisa wa usalama wakiuchukua mwili wa mtoto huyo aliyefanyiwa ukatili na mtu ambaye hajafahamika kwa sasa.
Kulingana na wazazi wa mtoto huyo Bernadict Keziah ambaye yuko gredi ya ya Pili, walimsaka usiku kucha katika sehemu mbali mbali bila mafanikio.
Familia hii inasema imeshtushwa na umati wa watu uliokuwa umekusanyika nje ya boma lao mapema asubuhi, wakati walipokuwa wanaendelea na juhudi za kumtafuta msichana wao.

Wakaazi wa Kwa Nzai eneo la Mwezang’ombe kaunti ya Kilifi wameghubikwa na wingu la majonzi baada ya mtoto wa miaka 7 kubakwa na kuuwawa
Babake msichana huyo Brandon Matuki pamoja na mamake Faith Namwezi wanasema walikuwa na matumaini makubwa na maisha ya mtoto huyo wa kipekee, waliyemtaja kama mpenda watu na mkakamavu masomoni wakitaka wahusika kutafutwa na kukabiliwa.
Baadhi ya majirani wa Karibu wa Familia hiyo wamekemea kitendo hicho cha kinyama, wakitaka viongozi bungeni kubuni sera za kukabiliana na wanaopatikana na hatia ya kutekeleza vitendo kama hivyo kwa watoto wadogo.
Mwili huo unahifadhiwa katika makafani ya Hospitali ya rufaa ya Kilifi mjini Kilifi, ukitarajiwa kufanyiwa upasuaji jumanne wiki hii huku maafisa wa polisi wakiendelea na uchunguzi wa mauaji hayo.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

