Connect with us

News

Bajeti ya taifa yawasilishwa bungeni kujadiliwa

Published

on

Bunge la kitaifa linatarajiwa kujadili hoja ya makadirio ya bajeti ya kitaifa ya mwaka wa 2026/2027 ya shilingi trilioni 4.79.

Kiongozi wa wengi katika bunge la kitaifa Kimani Ichung’wah aliwasilisha nakala ya bajeti hiyo bungeni ambayo imeongezeka na shilingi bilioni 65 ambayo ni sawa na asilimia 1.92, ikilinganishwa na bajeti ya mwaka wa 2025/2026.

Katika bajeti hiyo, Mamlaka ya ukusanyaji ushuru nchini KRA, inakadiria kukusanya takribani shilingi trilioni 3.629 ili kupiga jeki bajeti hiyo sawa na kufanikisha matumizi ya serikali na utekelezaji wa miradi ya maendeleo nchini.

Katika bajeti hiyo, serikali pia inalenga kukopa kima cha shilingi bilioni 995.7 kwa wawekezaji wa ndani kwa ndani ili kuchangia kufanikisha bajeti hiyo ambayo inaonekana kwamba uko juu zaidi.

Kwenye bajeti hiyo, hazina ya kitiafa inalenga sehemu ya ufadhili wa kibiashara kutoka nje ambao umepangiwa shilingi bilioni 145.6, jambo linaloashiria kurejea katika masoko ya kimataifa.

Bunge la kitaifa la Kenya laendelea na vikao vyake bungeni

Sekta ya barabara na uchukuzi imetengea shilingi bilioni 298.5, Tume ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC ikitengewa shilingi bilioni 25.4, sekta ya elimu ikitengewa shilingi bilioni 668.3, sekta ya usalama ikipangiwa shilingi bilioni 566.8, sekta ya afya ikitengewa shilingi bilioni 170.7 huku sekta ya Kilimo kipokea mgao wa shilingi bilioni 62.9.

Hata hiyo serikali za ugatuzi zimetengewa shilingi bilioni 420 licha ya serikali hizo kudai kwamba mgao huo ni mchache na kupendekeza shilingi bilioni 470, huku sekta ya mgao wa shilingi bilioni 9.6 ukitengwa kama mgao wa fedha za zaida.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending