News
Wakaazi waandamana kupinga mauaji ya mtoto Keziah Kilifi
Wakaazi pamoja na Wanaharakati wa kutetea haki za binadamu katika Kaunti ya Kilifi wameandamana wakitaka idara ya usalama kuharakisha uchunguzi kuhusu mauaji ya kinyama ya mtoto wa miaka saba anayedaiwa kunajisiwa kabla ya kunyongwa, kisha mwili wake kutupwa karibu na nyumbani kwao katika kijiji cha Kwa Nzai, eneo la Mwezang’ombe.
Waandamanaji hao waliokuwa wamejaa huzuni na ghadhabu walitembea kutoka eneo la tukio hadi afisi ya Kamishna wa Kaunti ya Kilifi wakitaka majibu kuhusu hatua iliyofikiwa katika uchunguzi huo pamoja na hatua zilizochukuliwa dhidi ya wahusika.

Wakaazi waandamana kushinikiza maafisa wa usalama kumtia nguvuni mshukiwa wa mauaji ya mtoto Keziah
Maafisa wa polisi wakiongozwa na Kamishna wa Kaunti Simon Mutisya waliwahakikishia wananchi kuwa mshukiwa mmoja tayari ametiwa mbaroni huku maafisa wa upelelezi kutoka idara ya DCI wakiendelea na uchunguzi wa kina ili kuhakikisha wote waliohusika wanakamatwa na kufikishwa mahakamani.
Maafisa hao pia waliwataka wananchi kudumisha utulivu na kuipa nafasi idara ya usalama kukamilisha uchunguzi, wakisisitiza kuwa haki itapatikana kwa familia ya mtoto huyo.
Hata hivyo, mkutano uliokuwa umepangwa kuwa wa amani na wa kutafuta suluhu uligeuka kwa muda baada ya baadhi ya vijana waliokuwa na hasira kuondoa hema lililokuwa limewekwa kwa ajili ya viongozi wa kisiasa kuwahutubia wananchi.
Taaridfa ya Elizabeth Mwende
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

