News
Rais Ruto aelekea Marekani kwa mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa
Rais William Ruto ameondoka nchini Jumamosi 20, Septemba 2025, kuhudhuria Mkutano Mkuu wa 80 wa Umoja wa Mataifa mjini New York, nchini Marekani.
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, msemaji wa Ikulu Hussein Mohamed alisema ajenda ya rais Ruto mjini New York itakuwa juu ya ushirikiano wa pande nyingi, kutetea mageuzi ya mfumo wa fedha duniani, na kutoa wito wa upatikanaji wa haki wa fedha za maendeleo kwa nchi zinazoendelea.
Pia rais atashinikiza mageuzi ya umoja wa Mataifa ili kujumuisha zaidi na kushughulikia changamoto za amani na usalama duniani, ikiwa ni pamoja na kuimarisha juhudi za amani katika matifa ya Sudan, Sudan Kusini, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Somalia na Haiti.
Katika baraza kuu, kiongozi wa taifa pia anatarajiwa kutetea uwakilishi wa Afrika katika baraza la usalama la umoja wa mataifa, ambapo bara hilo lina uanachama usio wa kudumu pekee.
Chini ya majadiliano ya kiserikali juu ya mageuzi ya baraza la usalama la umoja wa mataifa, nchi wanachama zinapigania ongezeko la viti vya kudumu na visivyo vya kudumu, ili kuwa uwakilishi wa kweli wa chombo hicho cha kimataifa.
Katika wiki hiyo ya ngazi ya juu, Kenya pia inatarajiwa kufanya mazungumzo kuhusu misheni ya msaada wa usalama wa kimataifa ya Haiti, miaka miwili baada ya kutumwa kwa wanajeshi wake kuongoza misheni hiyo.
Taarifa Ya Joseph Jira
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

