Connect with us

News

Rais Ruto amebuni jopo la kukabiliana na ufisadi

Published

on

Rais William Ruto amebuni jopokazi la pamoja linaloshirikisha idara mbalimbali nchini na mashirika ya kiserikali ili kupiga jeki vita dhidi ya ufisadi nchini.

Jopokazi hilo linahusisha asasi za kiusalama ikiwemo idara ya ujasusi nchini NIS, idara ya upepelezi wa jinai nchini DCI, Tume ya maadili na kupambana na ufisadi nchini EACC, na Ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka ya umma ODPP.

Taasisi zengine ni pamoja na Ofisi ya Mwanasheria mkuu, Mamlaka ya ukusanyaji ushuru nchini KRA, Benki kuu ya Kenya, Mamlaka ya ununuzi wa bidhaa za umma, Kituo cha kutoa taarifa za fedha na mamlaka ya urejeshaji wa mali ya umma.

Rais Ruto ambaye aliondoka humu nchini na kuelekea taifa la Japan kwa ziara ya siku tatu, amesema vita dhidi ya uvujaji wa mali ya umma ni lazima ukomeshwe kwani umeathiri pakubwa uchumi wa taifa.

Hatua hiyo ya rais imejiri siku moja baada ya kuwashambulia wabunge na maseneta, akidai kwamba baadhi yao wamekuwa wakishiriki ufisadi ili kuwasuru magavana pamoja na kupitisha miswada bungeni.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending