News
Rais Ruto ameita saini mswada wa kukabili utakatishaji Fedha
Rais William Ruto ametia saini kuwa sheria mswada wa kupambana na utakatishaji Fedha na kufanyia marekebisho sheria ya kupambana na ufadhili wa ugaidi ya 2025.
Mswada huo, uliofadhiliwa na Kiongozi wa walio wengi katika bunge la kitaifa Kimani Ichung’wah, ulilenga kuziba mianya ambayo imewezesha ufujaji wa pesa na mtiririko haramu wa kifedha, kupitia shughuli za kubadilishanaji raslimali.
Mswada huo ulifanyia marekebisho vipingee 10 vya sheria za bunge ili kukabiliana na mapungufu ya kiufundi ya uzingatiaji, yaliyobainishwa na kundi la kupambana na utakatishaji fedha haramu wa mashariki ya kusini mwa afrika (ESAAMLG).
Jopo la kifedha (FATF) linalojihusisha na harakati za kupambana na utakatishaji fedha haramu, kupambana na ufadhili wa ugaidi na kupambana na ufadhili wa kuenea pia yamehusishwa.

Rais Ruto na viongozi wa kiserikali wakati wa kutia saini mswada wa utakatishaji fedha
Sheria hizo zilizofanyiwa marekebisho ni pamoja na ile ya mapato ya uhalifu na kupambana na utakatishaji fedha haramu ibara ya 59 A, sheria ya kuzuia ugaidi ibara ya 59 B, na Sheria ya michezo ya kamari na bahati nasibu ibara ya 131, sheria ya mafao ya kustaafu sura ya 197.
Sheria nyengine ni ile ya madini sura ya 306, na sheria ya vyama vya ushirika ibara ya 490 B na sheria ya uhasibu ibara ya 531.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

