News
Rais Ruto asema serikali imeweka kwenye sekta ya Elimu na Afya
Rais William Ruto amesisitiza kuwa serikali yake inawekeza kwa kiwango kikubwa katika sekta muhimu za elimu na afya ili kuhakikisha maisha bora kwa wananchi.
Akizungumza katika Chuo Kikuu cha Umma, kaunti ya Kajiado, Rais Ruto alisema serikali imeongeza mgao wa fedha kwa vyuo vikuu kwa zaidi ya shilingi bilioni 130 ili kuinua kiwango cha elimu ya juu nchini. Alibainisha kuwa hatua hiyo inalenga kusaidia wanafunzi wengi zaidi kupata nafasi ya masomo na kuboresha ubora wa elimu.
Ruto aliongeza kuwa wanafunzi takriban 470 tayari wamenufaika na ufadhili na mikopo ya elimu kutoka serikali ya kitaifa. Aidha, alieleza kuwa vyuo vya kiufundi vimeimarika kwa kiwango kikubwa, na kupitia hamasa zinazofanyika kote nchini, idadi ya wanafunzi wanaojiunga na taasisi hizo imeongezeka maradufu. Rais alisema wanafunzi hao wanajipatia ujuzi muhimu utakaowasaidia kujiajiri na kukuza uchumi wa taifa siku zijazo.

Viongozi wahudhuri mkutano wa masuala ya elimu na afya uliogongwa na Rais William Ruto{Picha kwa hisani}
Kwa upande wake, Waziri wa Afya Aden Duale aliunga mkono kauli ya Rais akisisitiza kuwa serikali imepiga hatua kubwa katika mageuzi ya sekta ya afya. Duale alisema zaidi ya Wakenya milioni 26.5 tayari wamejiandikisha na Bima ya Afya ya Jamii (SHA) na kunufaika nayo, ikilinganishwa na milioni 7 pekee waliokuwa kwenye NHIF.
Waziri huyo alifafanua kuwa bima ya NHIF iliacha deni kubwa na haikuwajumuisha wananchi wote, tofauti na SHA inayolenga kila Mkenya. Duale pia aliwataka viongozi wa kisiasa kukoma kuingiza siasa katika sekta muhimu kama afya na elimu na badala yake kushirikiana na serikali katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora.
Taarifa ya Elizabeth Mwende
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

