Connect with us

News

Rais Ruto atia saini mswada wa fedha wa 2025 kuwa sheria.

Published

on

Rais William Ruto ameidhinisha Mswada wa Fedha wa 2025.

Ruto alitia saini mswada huo kuwa sheria asubuhi ya alhamisi tarehe 26 juni 2025 katika ikulu ya Nairobi baada ya wabunge kupitisha sheria iliyopendekezwa wiki jana.

Ingawa mswada huo uliepuka kuwasilisha ushuru mpya kufuatia maandamano mabaya ya mwaka jana dhidi ya mswada wa fedha wa 2024/2025, baadhi ya vifungu vilikuwa na utata kama vile pendekezo la kutaka kuipa Mamlaka ya kitaifa ya ukusanyaji ushuru KRA uwezo wa kufikia data ya kibinafsi na ya kifedha ya walipa kodi.

Wabunge hatimaye waliuangusha walipokuwa wakiupigia kura kabla ya kutumwa kwa rais Ruto ili kuidhinishwa.

Waziri wa hazina ya kitaifa John Mbadi aliwasilisha bajeti ya shilinghi trilioni 4.2 katika mwaka wa kifedha wa 2025/26 bungeni mapema mwezi huu, na wizara yake inatarajia kukusanya hadi shilingi bilioni 30 katika mapato ya ziada kutoka kwa mswada wa huo wa fedha.

Wakati huo huo, rais Ruto pia alitia saini mswada wa uidhinishaji wa mwaka 2025, utakaoruhusu hazina ya kitaifa kuchukua shilingi trilioni 1.88 kutoka kwa hazina ya pamoja kwa mwaka wa kifedha wa 2025/26.

Mswada huo unaruhusu wizara, idara na mashirika kutumia shilingi bilioni 672 katika ugavi wa msaada, kama ilivyoidhinishwa na bunge.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending