Connect with us

News

Rais Ruto awapongeza maafisa wa Polisi nchini

Published

on

Rais William Ruto ameahidi kuwaunga mkono maafisa wa polisi katika kutekeleza majukumu yao ya kulinda haki za kila mwananchi.

Rais Ruto alisisitiza haja ya kulinda pia Katiba ya Kenya pamoja na kulinda usalama wa Taifa, akisema hatua hiyo itachangia zaidi taifa kushuhudia amani na uzalendo.

Akizungumza katika Ikulu ya Nairobi siku ya Jumanne tarehe 24 Juni, 2025 Kiongozi wa taifa aliwapongeza maafisa wa polisi wakiongozwa na Inspecta Jenerali wa Polisi nchini Douglas Kanja akisema wamejitolea kuhakikisha taifa la Kenya linaishi kwa Amani.

Rais Ruto alisema viongozi wanaojaribu kuwatishia maafisa wa polisi wanapotekeleza shughuli zao hawawezi kudhalilisha kitengo cha polisi mbele ya macho yake.

“Kuna viongozi wengine wenye kukejeli maafisa wa polisi wanapotekeleza majukumu yao, hiyo haifai tuwape nafasi polisi wetu waendeleza kazi zao kwa kuzingatia sheria na kulinda wananchi bila ya kusumbuana kwa sababu Kenya ni yetu sisi sote”, alisema Rais.

Vile vile alipongeza juhudi za maafisa wa usalama kutoka nchini Kenya ambao wao nchini Haiti katika katika oparesheni ya Kiusalama kama njia moja wapo ya kuleta Amani nchini humo.

Picha kwa hisani

Kwa upande wake Inspekta Jenerali wa Polisi nchini Douglas Kanja, aliahidi kwamba maafisa wa polisi watatekeleza majukumu kwa kuzingatia sheria na mwongozi wa Katiba.

Haya yanajiri huku Wanaharakati wa kutetea haki za kibinaadamu pamoja na vijana wa kizazi cha Gen-z wakishiriki maandamano ya kupinga ukatili unaotekelezwa na maafisa wa polisi nchini.

Hata Juni 25 siku ya Jumatano, vijana wa Gen Z walidai kwamba watashiriki maandamano ya amani kushinikiza kuwajibika zaidi sawa na kuchukuliwa hatua kwa maafisa wa polisi wanaohusika na mauaji ya wananchi kiholela.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending