Connect with us

News

Sarai, amkosoa Waziri Murkomen kwa madai ya kuhujumu mashirika ya kiislamu

Published

on

Katibu mkuu wa Chama cha UDA Hassan Omar Sarai, imemkosoa Waziri wa usalama wa ndani Kipchumba Murkomen kutokana na kuchapisha katika gazeti rasmi la serikali kundi cha Muslim Brotherhood na Hizb-ur-Tahrir kama mashirika la kigaidi.

Sarai alisema hatua hiyo inahujumu jamii ya Waislamu nchini na hata katika mataifa ya ughaibuni, akisema ingekuwa bora zaidi iwapo serikali ingechapisha katika gazeti hilo kundi la Zionist la Israel kama Shirika la Kigaidi.

Sarai alipendekeza kufanyiwa marekebisho kwa sera za kimataifa za Kenya na kutoa wito wa kuwepo kwa uwiano thabiti na jamii ya kiislamu ulimwenguni huku akipinga uhusiano na taifa la Israel.

Wakati huo huo alisema Waziri Murkomen alitumia sera ya kudhibiti ugaidi ya mwaka wa 2025 kukandamiza mashirika hayo, na hivyo basi ni yeye pekee ndio mwenye uwezo ama Mahakama ya Kenya kuondoa chapisho hilo kwenye gazeti rasmi la serikali.

Hata hivyo alidokeza kwamba suala hilo limeangaziwa katika mataifa mbalimbali na huenda likachangia athari kubwa ya kiusalama kutokana na kuhusishwa kwa itakadi na vurugu.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending