News
Serikali kusambaza neti milioni 10 kwa wananchi kuzuia Malaria
Kenya inatarajia kusambaza neti za kuzuia Mbu milioni 10 kwa wananchi mashinani huku Wizara ya Afya nchini ikiimarisha juhudi za kudhibiti maambukizi na vifo vinavyotoka na ugonjwa wa Malaria.
Katibu katika Idara ya Afya ya umma nchini Mary Muthoni amesema Malaria bado ni changamoto kubwa kwa Afya ya umma, akisema visa milioni 4.2 vilirekodiwa mwaka wa 2024.
Muthoni alisema kuna haja ya kushirikisha kila mmoja katika juhudi za kudhibiti maambukizi ya Malaria nchini, akiwataka wananchi kusafisha mazingira yao ili kuwa na mazingira safi na salama kwa maisha yao.
“Tunapanga kusambaza zaidi ya vyandarua vya kuzuia Mbu milioni 10 kote nchini, kama hatua moja wapo ya kuzuia maambukizi ya Malaria na vifo kwani ugonjwa wa Malaria umekuwa changamoto kuu nchini”, alisema Muthoni.
Kwa upande wake mkuu wa mpango wa Malaria katika Wizara ya Afya nchini Dk Kibor Keitany alisema kiwango cha mamabukizi ya malaria nchini kimeshuka hadi asilimia 6 mwaka wa 2020 kutoka asilimia 8 mwaka wa 2025.
Keitany alisema mpango huo unalenga kupunguza Malaria kwa asilimia 80 na kupunguza vifo vinatokana na ugonjwa huo kwa asilimia 90.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Polisi kutumia nguvu kukabiliana na wahalifu
Huenda maafisa wa polisi wakutumia nguvu kupita kiasi katika kukabiliana na wahalifu ama wale wanaolenga kuzua vurugu na fujo mashinani.
Idara ya usalama nchini imesisitiza kwamba itakabiliana kikamilifu na magenge ya kihalifu ambayo yanaendeleza uhalifu mashinani na kutatiza shughuli za kibiashara, uchumi na usalama wa taifa.
Idara hiyo ilisema tayari imebaini magenge ya kihalifu ambayo yanatatiza usalama wa wananchi, huku wazazi wakilaumiwa kwa kuwatetea watoto wao licha ya kufahamu kwa tabia hiyo inazidi kuhatarisha maisha ya jamii mashinani.
Idara hiyo, ililalamikia kukithiri kwa utovu wa usalama hasa kaunti za Kwale, Mombasa na Lamu katika ukanda wa Pwani, kutokana na vijana wengi kuzama katika uraibu wa Mihadarati na ukosefu wa kazi, hatua iliyopelekea baadhi ya vijana kujiunga na magenge ya mapanga.
Kauli hiyo ya idara ya usalama ilijiri siku moja tu baada ya Kamanda wa Polisi kanda ya Pwani Ali Nuno, kuagiza maafisa wa polisi kuwapiga risasi magenge ya kihalifu ya vipanga kwa kutatiza usalama.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Mswada wa marekebisho ya Katiba wa mwaka 2026 umewasilishwa bungeni
Mswada wa marekebisho ya Katiba wa mwaka 2026 na sheria za uchaguzi umewasilishwa katika bunge la Seneti.
Mswada huo unalenga kufanyia marekebisho kipengele cha Katiba cha 99 na 193 pamoja na sheria za uchaguzi sehemu ya 24 na 25 ili kuwepo na uwazi kwa magavana wanaolenga kuwania nyadhfa za uongozi baada ya kukamilisha mihula yao.
Mswada huo uliowasilishwa na Seneta wa Kirinyaga James Murango unalenga pia kuzuia magavana waliomaliza mihula yao ya uongozi kutowania nyadhfa za useneta, ubunge ama uwakilishi wadi, kwani inakuwa vingumu kuchunguzwa.
Kuwasilishwa kwa mswada huo bungeni kufuatia hali magavana kuwania wadhfa wa useneta baada ya kukamilisha mihula yao ya uongozi hali ambayo imeleta sintofahamu ya kiuongozi, ikiashiria tamaa za uongozi na njama ya kuhitilafiana na ufuatiliaji wa matumizi ya raslimali za umma.
Seneta Murango alisema katika utekelezaji wa majukumu yao, magavana hulazimika kuwajibika mbele ya mabunge ya kaunti na Seneti kuhusu matumizi ya kifedha na kiutawala.
Wakati huo huo alidokeza kwamba iwapo mswada huo utapishwa na kuwa sheria utasaidia kufutilia usimamizi wa raslimali za kaunti na matumizi ya fedha kwani utazuia magavana kuhitilafiana na uchunguzi.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

