News
Serikali yaahidi kuboresha huduma za afya kupitia UHC.
Waziri wa afya, Aden Duale, amesema serikali imeweka mikakati dhabiti kuhakikisha kila mkenya anapata huduma bora za afya kupitia mpango wa bima ya afya kwa wote (UHC).
Akizungumza wakati wa kufungua kongamano la 45 la kisayansi la chama cha wanafamasia (PSK), Duale alibainisha kuwa hatua hizo ni pamoja na kuhakikisha upatikanaji wa dawa na bidhaa muhimu za afya kwa zaidi ya asilimia 80, kuboresha mifumo ya utoaji huduma, na kuimarisha matumizi ya teknolojia ya kidijitali ili kuongeza uwazi, tija na thamani ya matumizi ya fedha katika sekta ya afya.
Waziri Duale aidha alieleza kuwa serikali inaendelea kukeleza mpango wa kuanzisha hazina ya bima ya afya kwa jamii (SHA) ili kuhakikisha hakuna mwananchi anayeachwa nyuma, akisisitiza kwamba afya ni haki ya kikatiba na msingi wa maendeleo ya taifa.
Waziri Duale pia alitaja changamoto zinazokumba sekta ya mafunzo ya wataalamu wa afya, hasa kuibuka kwa taasisi za mafunzo ya famasia bila udhibiti madhubuti, hali aliyoitaja kuwa tishio kwa ubora wa elimu na huduma katika taaluma hiyo.
Kadhalika alibainisha kuwa utengenezaji wa dawa ndani ya nchi, kuboresha udhibiti kupitia bodi ya famasia na sumu (PPB), mfumo wa usambazaji wa dawa, kuimarisha usalama wa wagonjwa, na kujumuisha huduma za famasia katika mfumo wa bima ya afya ya kitaifa kuwa baadhi ya mambo yatakayopewa kipaumbele
Taarifa ya Mwanahabari wetu
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

