News
Serikali yatenga shilingi milioni 250 kwa Walemavu.
Serikali kupitia Wizara ya Leba na maslahi ya kijamii imetenga shilingi milioni 250 mwaka wa 2025 ili kuimarisha uwezeshaji wa watu wanaoishi na ulemavu nchini.
Katibu mkuu wa wizara hiyo Joseph Motari alitangaza kuwa ufadhili huo utasaidia masuala ya elimu, kuwawesha kiuchumi pamoja na teknolojia kwa jamii hiyo.
Motari alibainisha hayo wakati wa kikao cha 18 cha mkutano wa nchi wanachama wa mkataba wa haki za watu wenye ulemavu (CRPD) jijini New York nchini Marekani.
“Kenya inaongeza juhudi zake za kujumuisha uchumi kwa kutenga zaidi ya shilingi milioni 250 mwaka huu kupitia msaada wa elimu, uwezeshaji wa kiuchumi na msaada wa kiteknolojia”, Motari alisema.
Katibu huyo pia aliangazia utekelezaji wa mpangilio wa mkakati wa mwaka 2023-27 ambao unayapa kipaumbela masuala ya ufahamu, uwezeshaji wa kijamii na kiuchumi, vile vile ujumuishaji wa kidijitali kwa watu wanaoishi na ulemavu.
Kulingana na Motari, takribani makaazi elfu 63 yatanufaika na program za serikali za kusambaza pesa na upokezaji wa marupurupu ya kila mwezi ya shilingi elfu mbili.
Kati ya hao zaidi ya walengwa elfu 20 wanafadhiliwa chini ya mpango ujulikanao kama Autism and Developmental Disabilities programme.
Mwaka 2024, serikali ilisambaza takriban vifaa 4,200 vya usaidizi kwa jamii hiyo pamoja na kutoa ufadhili wa masomo kwa wanafunzi 2,500 wanaoishi na ulemavu.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

