News
Serikali yaweka wazi hatua ilizopiga chini ya uongozi wa Rais Ruto
Serikali imeweka wazi hatua ilizopiga katika kipindi cha miaka mitatu tangu Rais William Ruto achukue hatumu ya uongozi nchini.
Katika taarifa iliyotolewa na taifa kupitia vyombo vya habari na Msemaji wa serikali Isaac Mwaura, imeguasia baadhi ya vipengele vilivyoangaziwa na serikali katika kipindi cha miaka mitatu ambapo serikali imeonyesha mafanikio yake.
Katika sekta ya Utalii, serikali imesema utalii unakuwa kwa kasi kwani watalii wa kimataifa wanaowasili wakifikia milioni 2.42 na mapato kutoka kwa sekta hiyo kufikia shilingi bilioni 462.21.
Mwaura ameeleza kwamba ukuaji huu unadhihirisha juhudi za serikali katika kufufua utalii na kuhifadhi wa Wanyamapori na kuchangia kwa kiasi kikubwa katika pato la taifa na kuongeza ajira katika sekta hiyo.
Akigusia ukuaji wa uchumi wa taifa, Mwaura ameweka wazi kwamba serikali ina dhamira ya kuendeleza juhudi hizo chini ya mpango wa ajenda ya mabadiliko ya kiuchumi yaani Bottom up Economy Transformation Agenda {BETA}, akisema umechangia ajira kwa vijana, utoaji wa huduma, na uwezeshaji wa kiuchumi.
Wakati huo huo alifafanua kwamba huduma za afaya nchini zinaendelea kuwafikia wananchi mashinani, kwani wakenya milioni 25.8 tayari wamejisajili na Mamlaka ya afya ya jamii SHA kwnai zaidi ya wasimamizi wa afya ya jamii laki moja wamepokea mafunzo ya kutoa huduma mashinani.
Aidha kwenye sekta hiyo ya Afya, zaidi ya hospitali 350 zimejenhwa na kupandishwa vyeo huku vituo vya afya 10,582 vikiwekwa kwenye mfumo wa kidijitali ili kuimarisha utoaji wa huduma ikiwemo Saratani, magonjwa sugu miongoni mwa mengine.
Hata hivyo kwenye sekta ya Kilimo, serikali imepiga hatua kubwa katika kufufua kilimo hatua iliyosababisha kushuka kwa bei ya unga wa Mahindi kwa asilimia 34 na kuboresha upatikanaji wa chakula na zaidi ya wakulima milioni 7 wakisajiliwa katika hifadhi data ya kidijitali na mifuko milioni 21 ya mbolea imesambazwa nchini.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

