News
Sifuna atimuliwa kutoka wadhifa wake wa Katibu mkuu wa ODM
Seneta wa Nairobi Edwin Sifuna ametimuliwa kutoka wadhifa wake kama Katibu mkuu wa Chama cha ODM na nafasi yake kuchukuliwa na Catherine Omanyo.
Uamuzi huu umeafikiwa katika kikao maluum cha Kamati kuu ya Chama cha ODM kilichofanyika Februari 11 mjini Mombasa na kuongozwa na Kinara wa Chama hicho Dkt Oburu Oginga.
Hatua hiyo ambayo haikutarajiwa hivi karibuni ilizua gumzo na hisia mseto na kuzidisha mpasuko na joto la siasa ndani ya Chama cha ODM.
Ni dhahiri kwamba Edwin Sifuna sasa ataongoza mrengo wenye siasa kali ndani ya Chama hicho cha ODM kinachoungwa mkono na
Ruth Odinga,Winnie Odinga, Babu Owino, Caleb Amisi, James Orengo, Majimbo Kalasinga na Richard Onyonka.
Mzozo ndani ya Chama Cha ODM uliibuka baada ya Kifo cha mwasisi na Kinara wa Chama hicho Marehemu Raila Amollo Odinga kuhusu tofauti za mstakabali wa Chama.
Kinara wa sasa Oburu Odinga na wandani wake wanasititiza Chama kusalia kwenye mpango wa serikali jumuishi chini ya Rais William Ruto kwa kuheshimu wosia wa Marehemu Raila huku kambi inayoongozwa na Edwin Sifuna na Babu Owino ikipinga kauli hiyo.
Mrengo wa Kinara wa Chama hicho Oburu Odinga umekuwa ukiendelea kampeni ya Linda Ground huku Edwin Sifuna na James Orengo wakianzasha vuguvugu la ODM Lina Mwananchi na mkutano wa hivi punde ukiandaliwa Busia.
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

