Connect with us

News

Ukosefu wa hamasa kuhusu sheria ni changamoto kwa makundi ya wachache

Published

on

Mashirika mbali mbali ya kuangazia maslahi ya kijamii wameendelea kukongamana mjini Malindi katika kaunti ya Kilifi kujadili masuala ya haki na sheria miongoni mwa makundi tofauti katika jamii.

Katika siku ya Pili ya Kongamano hilo linaloongozwa na Shirika la Msalaba Mwekundu nchini, imebainika kuwa ukosefu wa hamasa kuhusu sheria miongoni mwa waraibu wa dawa za kulevya imekuwa changamoto miongoni mwao kujitetea wanapojikuta wameenda kinyume na sheria.

Abdhala Badlusi Mkurugenzi wa MEWA kitengo cha kusaidia waraibu hao, amesema hali hiyo imewaacha waraibu wengi kujikuta njia panda katika kupata haki.

Badhlus amesema sheria za nchi zinafaa kuangazia namna jamii hizo zitaweza kupata haki kama watu wengine, ili kuhakikisha kuna usawa katika jamii.

Vile vile suala la haki katika masuala ya afya limeangaziwa katika Kongamano hilo, wadau wakisema maafisa wa afya nyanjani wamekuwa na mchango mkubwa kuhamasisha jamii ya watu wanaoishi na virusi vinavosababisha ukimwi katika kufikia huduma za afya.

Mashirika mbali mbali ya kongamana mjini Malindi katika kaunti ya Kilifi kujadili masuala ya haki na sheria miongoni mwa makundi tofauti katika jamii.

Hata hivyo mawakili wa ngazi ya jamii maarufu Paralegals wanasema suala la unyanyapaa katika jamii limekuwa kikwazo kikubwa kwa makundi haya kuendelea na maisha ya kawaida, wakishinikiza jamii kuwakumbatia watu hao na kuwapa motisha.

Kauli za washikadau hao zimeunga mkono na Hakimu katika Mahakama ya Kilifi Ivy Wasike, akisema sheria inawajibisha kila mmoja kulinda haki za makundi ya wachache katika jamii ili kufikia huduma muhimu za kiserikali.

Hakimu Wasike vile vile ameitaka jamii kuhakikisha inawakubali walio katika makundi ya wachache, akisema changamoto za kimaisha zinazowakumba huenda ni kutokana na masuala mbali mbali ya kifamilia.

Kongamano hilo la Siku tatu linatarajiwa kukamilika Alhamisi hii.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Aisha Jumwa akihama rasmi chama cha UDA

Published

on

By

Mgombea wa kiti cha ugavana wa kaunti ya Kilifi Aisha Jumwa amekihama rasmi chama cha UDA, akisema atatangaza baadaye mwelekeo atakaochukua wa kisiasa.

Jumwa alitoa tangazo hilo katika kikao na Wanahabari kilichofanyika katika makaazi yake, eneo la Kakuyuni huko Malindi kaunti ya Kilifi leo siku ya Alhamis.

Hatua ya Jumwa ilijiri baada ya kuwepo na tetesi kwamba alikuwa na mipango ya kuhama chama hicho kutokana na sintofahamu za kisiasa ndani ya chama cha UDA kuhusu msimamo wake wa kisiasa wa kuwania nafasi ya ugavana wa Kilifi.

Jumwa alilalamika kwamba alikuwa akinyanyaswa na baadhi ya viongozi hata kutimuliwa katika Ikulu ya rais licha ya kupambana katika kampeni za rais Ruto mwaka wa 2022, akionekana kumlaumu rais Ruto kwa kutomjali tena hata baada ya kusimama na yeye kisiasa.

Kiongozi huyo alikashfu vikali kutengwa katika mikutano ya UDA licha ya kuwa mwandani wa rais Ruto na pamoja na kufanyikisha miradi ya serikali mashinani, akisema tangu atangaze mchakato wa kuwania kiti cha ugavana wa Kilifi mwaka wa 2027, amekuwa akipitia masaibu mengi.

Hii sio mara ya kwanza kwa Jumwa kukihama Chama cha UDA na kurejea kwenye chama hicho, lakini hatua aliyoichukua sasa itabadili masimamo wa kisiasa kaunti ya Kilifi.

Itakumbukwa kwamba Jumwa amekuwa mwandani wa karibu wa rais William Ruto, lakini hatua aliyoichukua huenda ikabadili msimamo wa kisiasa kaunti ya Kilifi na Pwani kwa jumla. 

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Mahakama ya Kilifi yaagiza kuzuiliwa Washukiwa 7 wa mauaji

Published

on

By

Mahakama ya Kilifi imeagiza kuzuiliwa kwa siku 14 washukiwa 7 wanaotuhmiwa kuhusika katika kifo cha mwanamke mmoja aliyekuwa na umri wa miaka 65, ambaye aliuwawa kwa tuhma za uchawi katika eneo la Malomani eneo bunge la Ganze kaunti ya Kilifi.

Washukiwa hao Gilbert Karisa Changawa, Selvestar Changawa Kahindi, Elizabeth Jackson Ngala, Dhahabu Kithi Kombe, Dzendere Palu Kalama, Agness Changawa na Kadzo Ngombo Bienge watazuiliwa katika kituo cha Bamba wakati uchunguzi ukiendelea.

Kulingana na Afisa mpelelezi kutoka kitengo cha DCI ameeleza mahakama kwamba ilikuwa mnamo tarehe 27 mwezi huu ambapo walipokea tarifa kwamba dama changawa alikuwa amekatwa kichwa na kuuwawa na watu wasiojulikana usiku huo.

Afisa mpelelezi pia ameeleza kuwa washukiwa ambao ni wanafamilia,siku kabla ya tukio husika walikuwa wameandaa kikao cha kudumisha Amani baada ya kifo kilichokuwa kimetokea kwa kijana mmoja mtoto wa mmoja kati ya washukiwa aliyefariki kaunti ya Mombasa baada ya kupigwa kwa tuhma za wizi.

Kutokana na kifo cha kijana huyo wanafamilia hao walimtuhmu dama kwamba ndiye aliyekuwa amemroga kijana huyo na kusababisha kifo hicho cha gafla, ambapo usiku huo Dama aliuwawa nyumbani kwake.

Washukiwa watarudishwa mahakamani tarehe 13 mwezi Agosti mwaka huu baada ya uchunguzi kukamilika.

Taarifa ya Teclar Yeri

Continue Reading

Trending