News
Usalama waimarishwa Mombasa msimu wa Ramadhan na Kwaresma
Kamishna wa kaunti ya Mombasa Mohamed Noor amewahakikishia wakaazi wa Mombasa usalama wa kutosha msimu huu wa mwezi mtukufu wa Ramadhan kwa waislamu pamoja na mfungo wa Kwaresma kwa wakristo.
Akizungumza na Wanahabari, Noor alisema kamati ya usalama kupitia Kamanda mkuu wa polisi eneo hilo imeweka mikakati thabiti kuhakikisha usalama unaimarishwa.
Noor alisema ratiba za maafisa wa usalama kushika doria za usiku na mchana imepangwa ili kuhakikisha maafisa wa usalama wa kutosha wanakuwa nyanjani kukabiliana na visa vyovyote vya utovu wa usalama.
Noor alitoa onyo kali kwa wale wote wanaonuia kufanya uhalifu, akisema kuwa watachukuliwa hatua kali za kisheria.
“Tumetoa onyo kwa watu ambao wanalenga kutekeleza uhalifu kwamba wakome ama watakabiliwa na mkono wa sheria”, alisema Noor.
Ni kauli iliyopigiwa upatu na Sheikh Juma Ngao ambaye amesema waislamu watakuwa wakifanya ibada za usiku jambo ambalo limepelekea shinikizo zake za kuitaka idara ya usalama kuwajibika vilivyo.
Taarifa ya Mwanahabari wetu
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

