News
Vijana eneo la Junju, Kilifi wavuna wasipopanda
Maafisa wa Idara ya utawala wa mkoa katika wadi ya Junju kaunti ya Kilifi imeonya wakaazi wa kijiji cha Mwembetsungu dhidi ya kuendekeza visa vya wizi.
Hii ni baada ya mwanamke mmoja kunusurika kifo mikononi mwa wakaazi waliokuwa na gadhabu baada ya kumfumania akiiba mahindi kwenye shamba moja kijijini humo.
Mzee wa Mtaa kwenye kijiji hicho Elijah Mbigo alisema visa vya wizi wa mahindi kijijini humo vimekithiri mno msimu huu, huku akitaja kufikia sasa zaidi ya mashamba matano yamevamiwa na mahindi kuibiwa.
Akiongea na coco fm, Mbigo aliweka wazi kwamba tayari mikakati ya kukabiliana na wizi huo imewekwa huku akiwataka wakaazi wa kijiji hicho kushirikiana ili kuhakikisha wanaotekeleza wizi huo wanapatikana na kuchukuliwa hatua kali za kisheria.
“Onyo ninatoa kila siku lakini bado halijazingati kwa sababu vijana hapa niwavivu hawataki vibarua, hata wakiitwa kazi mahali hawaendi, sasa hiyo inafanya mtaa umeharibika kwa sababu ya uvivu wa vijana”, alisema Mbigo.
Kauli yake iliungwa mkono na mzee wa nyumba kumi kwenye kijiji hicho Benson Mganga ambaye alisisitiza haja ya ushirikiano miongoni mwa wakaazi huku akitaka sheria kali kuchukuliwa endapo wanaotekeleza wizi huo watapatikana.
Taarifa ya Mwanahabari wetu.
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

