Connect with us

News

Vijana na akina mama hawashiriki vikao vya ukusanyaji maoni Kilifi

Published

on

Imebainika kuwa idadi kubwa ya wanawake na vijana katika kaunti ya Kilifi bado hawajahamasishwa vilivyo kuhusiana na masuala ya uongozi, uundaji wa bajeti na sera katika serikali za kaunti na serikali kuu.

Katika kikao cha uzinduzi wa mradi wa meaningful Engagement And Transformative Action ( META) ambacho kimeandaliwa na Shirika la Timiza Youth Initiative na kuwaleta pamoja wadau mbalimbali, viongozi wa kaunti ya Kilifi, waandishi wa habari, vijana na akina mama.

Kulingana na Mwenyekiti wa Shirika la Timiza Youth Initiative Brian Mundia, hatua ya kuwatenga vijana na akina mama pamoja na wadau mbalimbali katika kutoa maoni yao kuhusu miradi ya maendeleo kumechagia wengi wao kusalia nyuma katika masuala yanayohusu maendeleo, uongozi na matumizi ya mitandao.

Mundia alisema mradi huo ambao pia unawalenga watu walio na uatilifu, wanapania kuzuru hadi maeneo ya mashinani kuhakikisha kuna hamasa ya kutosha na namna ya kutumia mitandao ya kidijitali kujibunia nafasi za ajira na wanashirikiana na wizara ya jinsia ile ya ugatuzi na mazingira kaunti ya Kilifi ili kufanikisha suala hilo.

Kwa upande wake Jackline Waweru wa shirika la Leadership For Impact, alisisitiza umuhimu wa vijana na akina mama kuhamasishwa kuhusu umuhimu wa kushiriki upigaji wa kura ili kuwaepusha kutumiwa visivyo na wanasiasa.

Ni kauli ambazo ziliungwa mkono na Waziri wa ugatuzi kaunti ya Kilifi, Clara Chonga ambaye alisema wanaweka mikakati kuhakikisha Wananchi wa kaunti ya Kilifi wanaweza kushiriki zoezi la ukusanyaji wa maoni pia kupitia mfumo wa kidigitali.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending