News
Polisi watoa onyo kwa wanyakuzi wa ardhi Kilifi
Idara ya usalama kaunti ya Kilifi imetoa onyo kali kwa wanaoendeleza unyakuzi wa ardhi za umma, ikisema watakabiliwa kikamilifu.
Kamishna wa kaunti ya Kilifi David Wanyonyi ametoa onyo hilo, akizidi kulionya kundi la Team Mashamba dhidi ya tabia hiyo.
Katika kikao na Wanabahari kuhusu usalama wa kaunti ya Kilifi kabla ya ziara ya rais William Ruto ya uzinduzi wa miradi ya maendeleo, Wanyonyi amesema serikali haitalinyamazia suala hilo wakati wananchi wakiendelea kuhangaishwa.
Kamishna Wanyonyi alisema tayari maafisa wa usalama wako nyanjani kuhakikisha usalama unaimarishwa kabla ya ziara ya rais, akiwataka wananchi kuondoa wasiwasi kwani maafisa wa usalama wako imara kulinda mali na raslimali za wananchi.
“Kama maafisa wa usalama tunatoa onyo kwa wavamizi wa mashamba ya umma wakidhani hayatumiki, tunawaambia hiyo tabia waache, hasa hii Team Shamba imekuwa na tabia ya kuvamia mashamba na kugawa, tunawaambia hiyo tabia hatutakubali na kutawakamata”, alisema Wanyonyi.
Aidha alisisitiza kwamba maafisa wa usalama hawatarudi nyuma katika kupambana na walanguzi wa dawa za kulevya kaunti ya Kilifi, akisema watakamatwa na kufikishwa Mahakamani ili kulinda vijana dhidi ya Mihadarati.
“Ni kweli kumekuwa na kesi za Mihadarati, lakini tunasema kwamba kama maafisa wa usalama kwa ushirikiano na vitengo mbalimbali tutahakikisha walanguzi wa Mihadarati wamekamatwa na kufikisha Mahakamani kulingana na sheria’,alisisitiza Wanyonyi.
Ziara ya rais Ruto kanda ya Pwani inatarajiwa kuwa na manafaa makubwa kwa wananchi, huku suala tata la ardhi, likitarajiwa kuangaziwa na wananchi kupewa hati miliki.
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

