Connect with us

News

Viongozi wa dini wamkosoa Kithure Kindiki.

Published

on

Viongozi wa dini ukanda wa wamemkosoa naibu rais profesa Kithure Kindiki kuhusiana na kauli yake kwamba baadhi ya viongozi wa dini na wanadiplomasia walihusika katika kuunga mkono maandamano ya vijana wa kizazi cha Gen Z ya mwezi juni 25 2025.

Mwenyekiti wa kitaifa wa baraza la kuu la waislamu SUPKEM Sheik Muhdhar Khitamy alisema matamshi ya Kindiki ni siasa zinazolenga kuwanyooshea lawama viongozi wengine.

Sheikh Kitamy alisema kuwa kwa sasa wanasiasa wamekuwa na usemi mkubwa kutokana na hulka ya kuwahonga wananchi na kuwafanya viongozi wa dini kutosikizwa.

Akizungumza na wanahabari kiongozi huyo wa dini ya kiislamu alionya kuwa  iwapo wakenya hawatakuwa makini, kunauwezekano wa taifa kuelekea pabaya kutokana na vijana kutumiwa vibaya na wanasiasa.

“Ukweli wa mambo ni kwamba wanasiasa wanachukuwa jukumu kubwa sana kwa sababu ya pesa za kuwatumia watu, jambo lolote liwe la kikatiba au nini utaona linawahusisha hao wanasiasa, twawaambia wanasiasa hao ndio chumvi, watengeneze nchi, watakuja kujuta kwasababu hali inavyokwenda ni mbaya”, alisema Khitamy.

Naye mwakilishi wa vijana katika baraza hilo Abdhulmalik Ali aliwataka vijana nchini kuwa makini na kufuata ushauri wa kisheria iwapo hawajaridhishwa na utendakazi wa viongozi.

Ali vile vile aliwashinikiza vijana kuepuka maandamano ya vurugu.

“Wanasiasa tuchungane nao, niwatu wanamaslahi yao zaidi ya wewe kijana, hii kenya inakuhitaji wewe kijana, kama kiongozi anatufaa tumpigie kura muhula ujao, kama hatufai njia iko ya kumtoa lakini sio suala la kumwaga damu”, alisema Abdhulmalik.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Rais Ruto atia saini kuwa sheria mswada wa hazina ya uwekezaji wa mali

Published

on

By

Rais William Ruto ametia saini kuwa sheria mswada wa hazina ya kitaifa ya uwekezaji wa mali (Sovereign Wealth Fund), hatua inayotajwa kuwa muhimu katika juhudi za Kenya za kuimarisha usimamizi wa fedha za umma, kulinda utajiri wa taifa na kuchochea ukuaji wa uchumi wa muda mrefu.

Utiaji huo wa saini ulifanyika katika Ikulu ya Nairobi na unaweka msingi wa kisheria wa kuanzishwa na kusimamiwa kwa mfuko wa taifa wa uwekezaji wa mali na kwamba unatarajiwa kuiwezesha nchi kuhifadhi rasilimali za umma zinazobaki baada ya matumizi ya kawaida, kufadhili uwekezaji wa kimkakati na kuimarisha uwezo wa uchumi kukabiliana na misukosuko ya kifedha siku zijazo.

Sheria hiyo mpya inaleta mfumo rasmi wa usimamizi wa utajiri wa taifa kwa kutenga akiba kwa ajili ya vizazi vijavyo, kuimarisha uthabiti wa uchumi na kufadhili uwekezaji katika miundombinu ya kimkakati ili kuongeza uimara wa kifedha nchini pamoja na kuhimiza matumizi yenye uwajibikaji ya rasilimali za umma.

Mfuko huo utatumika kuwekeza mapato ya ziada yanayotokana na rasilimali za asili na mali nyingine za umma, kwa lengo la kuhakikisha manufaa yake yanawanufaisha wananchi wa sasa na vizazi vijavyo.

Aidha, mfuko huo unakusudia kupunguza athari za changamoto za kiuchumi kwa kutoa kinga ya kifedha wakati wa misukosuko ya uchumi.

Sheria hiyo ni sehemu ya ajenda pana ya serikali ya mageuzi ya uchumi inayolenga kuimarisha usimamizi wa fedha za umma, kuongeza uwazi na kuendeleza maendeleo endelevu.

Pia, sheria hiyo imeweka mfumo wa uongozi na usimamizi wa mfuko huo, ukiwemo utaratibu wa kuhakikisha uwajibikaji, uwazi na usimamizi madhubuti katika uwekezaji na matumizi ya rasilimali za umma.

Maafisa wa serikali wameeleza kuwa Mfuko wa Taifa wa Uwekezaji wa Mali utakuwa na mchango mkubwa katika kufadhili miradi ya maendeleo yenye kipaumbele nchini huku ukihifadhi utajiri wa taifa kwa manufaa ya vizazi vijavyo.

Kupitishwa kwa sheria hiyo kunaiweka Kenya miongoni mwa mataifa yanayoongezeka duniani ambayo yameanzisha mifuko ya taifa ya uwekezaji wa mali kwa lengo la kulinda mali za taifa, kuimarisha uthabiti wa uchumi na kufadhili malengo ya maendeleo ya muda mrefu.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

IEBC yakosolewa dhidi ya masharti mapya kwa wanasiasa

Published

on

By

Kiongozi wa vijana katika Chama cha Wiper kaunti ya Kwale Nyawa Masai ameikosoa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC kutokana na masharti mapya iliyotoa dhidi ya wanasaisa kabla ya uchaguzi mkuu ujao.

Nyawa ameitaka Tume hiyo kuzingatia kanuni zake na taratibu za kuandaa uchaguzi na wala sio kila uchao kutoa masharti ambayo yanakinzana na majukumu ya Tume, akisema kuna taasisi zengine za umma zinafaa kuwajibika.

Akizungumza katika mkutano wa kisiasa katika eneo la Mwereni gatuzi dogo la Lungalunga kaunti ya Kwale, Nyawa aliesisitiza haja ya wanasiasa kupewa nafasi ya kuzungumza na wananchi sawa na kueleza sera zao bila ya vizuizi.

Kiongozi huyo wa vijana ambaye alitangaza nia yake ya kuwania kiti cha uwakilishi wadi ya Mwereni wakati wa uchaguzi ujao, amesema taifa la Kenya linazingatia demokrasia na kwamba kila taasisi inafaa kutekeleza majukumu yake.

“Katika uwaja wa siasa IEBC inakuzi moja tu kama msimamizi na kama msimamizi anaanza kutengeza sheria hapo ndipo anakosea, hii Kneya ni nchi ya demokrasia kwa hivyo IEBC isilete sheria nyingi na kufuatilia wanasiasa kuhusu pesa watatumia kwa kampeni, hiyo sio jukumu lake kuna taasisi inaitwa EACC”, alisema Nyawa.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending