News
Wahadhiri wa vyuo vikuu nchini wasitisha mgomo
Viongozi wa Muungano wa Wahadhiri wa vyuo vikuu nchini UASU na wale wa Wafanyikazi wa vyuo vikuu KUSU wamekubaliana kusitisha mgomo wao uliyodumu kwa takriban siku 49.
Viongozi hao wakiongozwa na Katibu mkuu wa Muungano wa UASU Constantine Wasonga walisema wamesitisha mgomo huo baada ya kuafikiana masuala kadhaa ambayo serikali ilikuwa bado haijaweka wazi.
Viongozi hao waliwaagiza wahadhiri wote wa vyuo vikuu na wale wa wafanyikazi kurejea kazini mara moja kuanzia siku ya Jumatatu ili kuendelea na masomo.
Katika kikao na Wanahabari baada ya mazungumzo na viongozi wa serikali yaliodumu kwa masaa kadhaa, Wasonga alisema wamekubali pendekezo la serikali la kuwalipa malimbikizi ya fedha zao kwa awamu mbili.
Aidha walisema wameafikiana kwamba kati ya shilingi bilioni 7.9 ambazo walikuwa wakidai serikali kulingana na mkataba wa makubaliano wa CBA, shilingi bilioni 3.8 zitalipwa mwezi Novemba na shilingi bilioni 3.8 zengine zikilipwa mwezi Juni mwaka 2026.
Kwa upande wake Waziri wa elimu nchini Julius Migos Ogamba alisema serikali itatimiza ahadi iliyoweka kwa wahadhari hao, akisema mkataba uliyotiwa saini kati ya serikali na viongozi wa vyama vya wahadhiri utatekelezwa kikamilifu.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

