Connect with us

News

Wahadhiri wa vyuo vikuu vya umma waapa kuendelea na mgomo

Published

on

Shughuli za masomo katika vyuo vikuu vya umma nchini zinaendelea kuathirika huku mgomo wa kitaifa wa wahadhiri ukiingia siku ya tatu leo.

Katibu mkuu wa chama cha wadhiri katika chuo kikuu cha pwani UASU Chris Ng’eny alisema serikali imekataa kuafikia mkataba wa maelewano wa mwaka 2017/2021 ambapo wanadai serikali shilingi bilioni 5.5.

Vile vile Ng’eny alisema kuna mikataba mingine ambayo serikali walielewana, japo kufikia sasa haijatekelezwa na wataendelea kususuia masomo hadi hatua zitakapochukuliwa.

Katibu huyo akizungumza na Coco Fm Ng’eny alisema serikali imekuwa ikitumia mbinu za uongo kushawishi wahadhiri kurejea madarasani kundelea na shughuli zao, japo hilo hawatalikubali.

“Serikali inatumia uongo sana, tarehe 15, waziri wa elimu aliandika barua kwa katibu wetu mkuu Daktari Constantine Wesonga kwamba wameachilia pesa shilingi bilioni 2.50 lakini hiyo pesa hatujaiona, jana wameandika taarifa kwa vyombo vyahabari kwamba wametoa pesa yote shilingi bilioni 2.73 lakini hayo yote ni uongo, tunasubiri kuona hiyo pesa mahali iko hatujaiona ndio maana tuko kwa mgomo”,alisema Ng’eny.

Kwa upande wake mwekahazina katika chama watetezi wa wafanyikazi katika chuo kikuu cha Pwani- KUSU, Saidi Kaonge, alishinikiza serikali kutekeleza lalama za wahadhiri baada ya mazungumzo ya awali, huku akitilia shaka iwapo serikali itaitisha mazungumzo mengine.

“Tumekubaliana na hao wacha watulipe kwa awamu kwa sababu walisema kwamba hawana pesa yakutosha, awamu ya kwanza wakalipa, awamu ya pili ndio hii nataka ufahamu ya kwamba hii awamu niyamakubaliano ya mwaka 2021/25 sasa hii ni awamu ya kwanza, awamu ya pili ya malipo ya hayo makubaliano ya mwaka 2021/21 inatakiwa ilipwe mwaka ujao 2026/27 sasa wasiwasi wetu ni kwamba iwapo haya marupurupu ya awamu ya kwanza hamtulipi je hayo marupurupu yajayo tutayafuatilia kwa njia gani”, alisema Kaonge.

Mgomo huo umeathiri wanafunzi wengi nchini hasa wanafunzi wanaojiunga na vyuo hivyo kwa mara ya kwanza.

Taarifa ya Joseph Jira

 

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending