Connect with us

News

Wakaazi wafunga ofisi ya Mwakilishi wadi wa Bamba kwa kukosa maji

Published

on

Tatizo la uhaba wa maji katika kaunti ya Kilifi limeendelea kugonga vichwa vya habari, bila ya kupata suluhu la tatizo hilo la mda mrefu.

Hii ni baada ya wakaazi kulalamikia kukosa maji kwa mda mrefu na kuchangia maandamano, ya vipi punde ikiwa ni wakaazi wa Bamba eneo bunge la Ganze, ambao katika maandamano yao walifunga ofisi ya Mwakilishi wadi ya Bamba Mohammed Mwambire.

Purukushani, mivutano na hatimaye vurugu, zilishuhudiwa nje ya ofisi ya Mwakilishi wadi hiyo na kusababisha wengine kupata majeruhisa.

Wakaazi hao walisisitiza kwamba ni lazima serikali ya kaunti ya Kilifi kupitia Mwakilishi wadi wao kuhakikisha eneo hilo la Bamba linapata huduma bora za maji safi kwa matumizi kwani wamehangaika kwa mda mrefu ama wataendelea na maandamano.

Mapema siku ya Alhamis Oktoba 23, Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro alililaumu shirika la usambazaji maji kanda ya Pwani kutokana na uhaba wa maji unaoshuhudiwa pamoja na kukarabati visima vya maji vilivyoharibika.

Akijibu lalama hizo zilizoibuliwa na serikali ya kaunti ya Kilifi kuhusu changamoto za maji, Mwenyekiti wa Shirika la huduma za usambazaji maji kanda ya Pwani, Dkt Daniel Mwaringa alikosoa kauli zilizotolewa na viongozi wa serikali hiyo, akisema Shirika hilo kukatiza huduma za maji kaunti ya Kilifi ni kutokana na kaunti hiyo kushindwa kulipa malimbikizi ya madeni kwa wakati.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending