News
Wakili George Kithi atambuliwa kama shujaa kwenye tuzo za kitaifa za Jamhuri, 2025
Kamati ya kitaifa kuhusu tuzo za Jamhuri imempongeza Wakili George Kithi kwa kutambuliwa kama shujaa wa afya, haki na masuala yanayoathiri jamii kwenye tuzo za kitaifa za mwaka 2025.
Utambuzi huu wa kifahari unasherehekea kujitolea kwake katika kupigania haki, maendeleo ya afya, na uongozi wa jamii unaoleta mabadiliko.
Kamati hiyo ilimtaja Kithi kama mwanasheria aliyebobea katika utumishi wa umma na mwenye huruma, na ambaye ameonyesha mara kwa mara kwamba uongozi hauhusu cheo, bali madhumuni na huduma zinazofaidi jamii.
Imetaja juhudi za wakili huyo katika kuboresha upatikanaji wa hudumu bora za afya, kusaidia programu za matibabu za kijamii, na kuwawezesha wanawake na vijana katika kaunti ya Kilifi kama zinazogusa maisha mengi.

Wakili George Kithi akisaidia mgonjwa aliyefika kusaka matibabu wakati wa kambi ya wiki ya matibabu ya bila malipo katika chuo kikuu cha pwani mjini Kilifi.
Kupitia wakfu wa George Kithi Foundation, kamati hiyo ilidokeza kuwa matumaini ya wengi na ndoto zilizohamasishwa vimerejeshwa na kukuza kizazi kipya cha wakazi wanaoendeshwa na malengo.
Katika sekta ya sheria, Kithi ametajwa kusimama kidete kwa usawa, ukweli, na uwajibikaji, sifa zinazoendelea kutia imani katika maono yake ya kuweko na Kilifi bora na jumuishi zaidi.

Wakili George Kithi akitangamana na baadhi ya wakaazi kwenye kambi ya wiki ya matibabu ya bila malipo katika chuo kikuu cha pwani mjini Kilifi.
Wamesifia utendakazi wake kama unaoziba pengo kati ya sheria, uongozi na ubinadamu unaoendelea kuunda safari yake na kuwatia moyo wengi kote nchini.
“Tuzo hii ya mwaka 2025 inasimama kama utambuzi wa kitaifa wa ujasiri wako, huruma, na kujitolea kwa mabadiliko ya umma”. imesema taarifa ya kamati hiyo.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

