News
Watu wawili wakamatwa kwa kumlaghai mtalii shilingi laki nane Mombasa
Maafisa wa upelelezi eneo la Nyali, kaunti ya Mombasa, wamemkamata mwanamke anayedaiwa kupanga njama ya wizi dhidi ya mpenzi wake raia wa uingereza baada ya kumwalika nyumbani kwake.
Mshukiwa huyo, Samira Mumbi Kiarie almaarufu Samira, anadaiwa kumlaghai mwingereza huyo kwa miezi kadhaa mtandaoni kabla ya kupanga njama ya kumvutia katika nyumba yake eneo la Nyali.
Kwa mujibu wa maafisa wa DCI, dakika chache baada ya mwanaume huyo kuingia ndani, wanaume wawili walivamia nyumba hiyo mmoja akijitambulisha kama mume wa Samira na mwingine kama afisa wa polisi.
Inasemekama walimtishia raia huyo na kumlazimisha kuhamisha zaidi ya shilingi laki nane kupitia simu kabla ya kutoweka.
Hata hivyo, baada ya uchunguzi wa kina wa kijasusi, maafisa wa DCI walifanikiwa kumtia mbaroni Samira pamoja na mshirika wake Paul Webster Mangeni, maarufu Paulo.
Ilibainika kuwa wawili hao ni sehemu ya genge linalowalenga wageni kupitia mitandao ya kijamii na kuwaibia.
Watuhumiwa hao wanazuiliwa katika kituo cha polisi cha Nyali wakisubiri kufikishwa mahakamani huku msako ukiendelea kumtafuta mshukiwa mwingine aliyetoroka.
Taarifa ya Mwanahabari wetu.
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

