Connect with us

News

Wanaharakati wa kijamii Kenya waahidi kuwatetea watanzania kutafuta haki

Published

on

Wanaharakati wa kutetea haki za kibinadamu nchini Kenya yameitaka Serikali ya Tanzania kusikiliza matakwa ya wananchi wake badala ya kuwatishia kukabiliana nao kikamilifu wakati wakipanga kufanya maandamano ya amani.

Wakiongozwa na Mkurugenzi mkuu wa Shirika la Vocal Africa Hussein Khalid, Wanaharakati hao walisema watanzania wamekuwa wakiandamana kwa amani na kulilia haki yao lakini serikali ya Tanzania imekuwa ikiwajibu kwa kuwakandama.

Khalid aliwataka watanzania kutorudi nyuma katika kutafuta haki yao, akisema kama watetezi wa haki za kibinadamu katika kanda ya Afrika Mashariki watasimama na watanzania katika kutetea haki yao.

“Sisi kama Watetezi wa haki za kibinadamu tutasimama na watanzania katika kupigania haki yao, na kwamba ni haki ya kila mmoja kuishi kwa amani lakini serikali ya Mama Samia imekuwa ikiwajibu watanzania wanaojitokeza kuandamana kwa amani kwa kuwashambulia na hata wengine kuuwawa”, alisema Khalid.

Kwa upande wake Afisa wa kitengo cha dharura wa Shirika la MUHURI Francis Auma alidai kwamba licha ya kushuhudiwa kwa mauaji nchini Tanzania, serikali ya taifa hilo haijawachukuli sheria waliotekeleza uhalifu huo.

“Ripoti zilionyesha wazi kwamba watu waliouwawa Tanzania ni zaidi ya watu elfu nne na tunashangaa hii serikali ya Mama Samia kwani nini imekosa utu, ni lazima watanzania wapigania haki yao na kukomesha unyanyasaji”, alisema Auma.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending