News
KNCHR yatoa ripoti ya ukiukaji wa haki za kibinadamu nchini
Tume ya kitaifa ya kutetea haki za kibindamu nchini KNCHR imesema zaidi ya watu 57 walipitia mateso na hata maafa katika hali tatanishi, mwaka huu wa 2025 pekee.
Tume hiyo ilitoa ripoti yake ya kila mwaka, ambapo ilibainisha kwamba mwaka huu pekee kumekuwa na visa 661 vya ukiukaji wa haki za binadamu.
Mwenyekiti wa Tume hiyo Claris Ogangah alisema maafisa wa tume hiyo walibaini kwamba uchaguzi mdogo wa Novemba 27 haukuwa huru na haki na kwamba katika maeneo ya Kasipul uchaguzi huo ulishuhudia maafa ya watu wawili.
“Katika kipindi tulichoandaa ripoti hii, Tume imebaini kupokea jumla ya malalamishi 2,848. Miongozi ya malalamishi hayo ni poamoja na ukiukaji wa haki za kibinadamu”, alisema Ogangah.
Akisoma ripoti hiyo Kamishna wa Tume hiyo Prof Marion Mutugi amesema uchaguzi huo mdogo ulishuhudia pia uwizi wa kura, kwani maafisa wa Tume hiyo ambao walikuwa waangalizi wa uchaguzi walinyima nafasi ya kufuatilia uchaguzi huo.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

