Connect with us

News

Wanaharakati wapinga ndoa ya jinsia moja Mombasa

Published

on

Vuguvugu la kupinga mahusiano ya jinsia moja mjini Mombasa limelalamikia bondi wanazopewa washukiwa wa kesi za ulawiti, wakisema pesa hizo huwa ni chache mno hali ambayo husababisha wanaotekeleza vitendo vya ulawiti huzidisha uovu huo.
Mwenyekiti wa vuguvugu hilo Salim Karama alisema hali hiyo imewafanya washukiwa wa ulawiti kuachiliwa kirahisi, wakitaka marekebisho kufanywa kwa vipengee vya kisheria ili kupunguza na hata kukomesha visa hivyo.
Karama aliitaka Idara ya Mahakama kuzichukulia kesi hizo kwa uzito ili kulinda kizazi kichanga kwani visa hivyo vinapoongezeka ni chanzo cha kupoteza kwa jamii na vijana wadogo ambao wanafaa kuwa mstari wa mbele kuchangia malengo elndelevu ya taifa sawa na kuheshimu mafunzo ya mwenyezi Mungu.
“Tunaitaka idara ya Mahakama nchini kuwa mstari wa mbele kukemea uovu huo pamoja na kuhakikisha haki kwa wale wanaotendewa unyama huo na kama Vuguvugu la kupinga mahusiano ya jinsia moja tutaendelea na shinikizo zetu kupinga uhalifu huu kwani sisi tunafaa wazi kwamba Ndoa ni mume na mke”, alisema Karama.
Wakati huo huo vuguvugu hilo liliahidi kuendelea kupinga dhulma za kingono na kutaka jamii kujitokeza na kuripoti visa hivyo ili kuwalinda watoto dhidi ya uovu huo.
Kauli hizo zilijiri baada ya Mahamakama kumuachilia jamaa mmoja anayedaiwa kumlawiti kijana wa miaka 12 kwa dhamana ya shilingi nusu milioni wakisema dhamana hiyo ni ndogo mno.
Taarifa ya Mwanahabari wetu
Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending