Connect with us

News

Wataalam wa uchumi samawati wakataa matumizi ya “Ring Net”

Published

on

Wataalam wa maswala ya uchimi wa bahari nchini wamesistiza marufuku ya uvuvi wa kutumia nyavu aina ya Ring Net wakisema nyavu hizo zinaharibu zao la samaki baharini.

Wakiongozwa na Stanley Chai, wataalam hao walisema nyavu hizo zinafaa kutumika kuanzia umbali wa maili tano baharini kutoka ufuoni hali ambayo wavuvi wa kawaida hapa nchini kwa sasa hawana uwezo wa kufika umbali huo.

Chai alidokeza kuwa nyavu hizo zinapotumika hunasa mayai ya samaki baharini hali inayosambaratisha na kuharibu kizazi cha viumbe hai baharini.

“Watu wetu hawa wavuvi wadogo wadogo wanatumia ndoana, uvuvi wa ring net nitakwambia si uvuvi mzuri hasa kama utakuja kwa maji yasiyo ya kina kirefu, ring net inabeba mpaka mayai ya samaki, ukiona nakala ya sheria zetu ambazo hazijachapishwa kwenye gazeti rasmi la serikali tumesema uvuvi wa ring net uruhusiwe umbali wa maili tano kuendelea na sio chini ya hapo kwa sababu chini ya hapo ndio samaki huzaana”, alisema Chai

Wakati huo huo Chai alisistiza umuhimu wa utekelezaji mpango wa kuingiza samaki nchini kutoka mataifa ya nje ili kuongeza kipato kupitia kodi na kuwezesha wavuvi kwa vifaa bora vya kuendeleza shughuli zao baharini.

“Wale samaki wakubwa tukiwaingiza hapa nchini tusiliseni ile ya dola elfu hamsini, hiyo ni kitu kidogo, yule samaki akiingizwa hapa nchini tunakusanya mabilioni, sasa hizi mabilioni tumesema nini kwa zile nakala ya sheria? tumesema zile pesa zitakazopatikana kwa biashara ya samaki asilimia 70 ziende kwa serikali kuu, asilimia 20 ziende kwa kaunti zinazopakana na bahari hindi, hii asilimia 10 iekezwe kuboresha wavuvi wadogowadogo halafu asilimia 10 ziende kwa vikundi vya maendeleo baharini-BMU, wale wavuvi moja kwa moja wanaweza kununua maboti makubwa nakupata uwezo wa kwenda kule chini”, aliongeza mtaalam Chai.

Kwa mda wavuvi eneo la pwani wamekuwa wakilalamikia serikali kuwafadhili na vifaa vya kisasa vya uvuvi ikiwepo boti zinazostahamili mawimbi baharini ili waweze kufika maji makuu na kuongeza pato la samaki.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Rais Ruto atia saini kuwa sheria mswada wa hazina ya uwekezaji wa mali

Published

on

By

Rais William Ruto ametia saini kuwa sheria mswada wa hazina ya kitaifa ya uwekezaji wa mali (Sovereign Wealth Fund), hatua inayotajwa kuwa muhimu katika juhudi za Kenya za kuimarisha usimamizi wa fedha za umma, kulinda utajiri wa taifa na kuchochea ukuaji wa uchumi wa muda mrefu.

Utiaji huo wa saini ulifanyika katika Ikulu ya Nairobi na unaweka msingi wa kisheria wa kuanzishwa na kusimamiwa kwa mfuko wa taifa wa uwekezaji wa mali na kwamba unatarajiwa kuiwezesha nchi kuhifadhi rasilimali za umma zinazobaki baada ya matumizi ya kawaida, kufadhili uwekezaji wa kimkakati na kuimarisha uwezo wa uchumi kukabiliana na misukosuko ya kifedha siku zijazo.

Sheria hiyo mpya inaleta mfumo rasmi wa usimamizi wa utajiri wa taifa kwa kutenga akiba kwa ajili ya vizazi vijavyo, kuimarisha uthabiti wa uchumi na kufadhili uwekezaji katika miundombinu ya kimkakati ili kuongeza uimara wa kifedha nchini pamoja na kuhimiza matumizi yenye uwajibikaji ya rasilimali za umma.

Mfuko huo utatumika kuwekeza mapato ya ziada yanayotokana na rasilimali za asili na mali nyingine za umma, kwa lengo la kuhakikisha manufaa yake yanawanufaisha wananchi wa sasa na vizazi vijavyo.

Aidha, mfuko huo unakusudia kupunguza athari za changamoto za kiuchumi kwa kutoa kinga ya kifedha wakati wa misukosuko ya uchumi.

Sheria hiyo ni sehemu ya ajenda pana ya serikali ya mageuzi ya uchumi inayolenga kuimarisha usimamizi wa fedha za umma, kuongeza uwazi na kuendeleza maendeleo endelevu.

Pia, sheria hiyo imeweka mfumo wa uongozi na usimamizi wa mfuko huo, ukiwemo utaratibu wa kuhakikisha uwajibikaji, uwazi na usimamizi madhubuti katika uwekezaji na matumizi ya rasilimali za umma.

Maafisa wa serikali wameeleza kuwa Mfuko wa Taifa wa Uwekezaji wa Mali utakuwa na mchango mkubwa katika kufadhili miradi ya maendeleo yenye kipaumbele nchini huku ukihifadhi utajiri wa taifa kwa manufaa ya vizazi vijavyo.

Kupitishwa kwa sheria hiyo kunaiweka Kenya miongoni mwa mataifa yanayoongezeka duniani ambayo yameanzisha mifuko ya taifa ya uwekezaji wa mali kwa lengo la kulinda mali za taifa, kuimarisha uthabiti wa uchumi na kufadhili malengo ya maendeleo ya muda mrefu.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

IEBC yakosolewa dhidi ya masharti mapya kwa wanasiasa

Published

on

By

Kiongozi wa vijana katika Chama cha Wiper kaunti ya Kwale Nyawa Masai ameikosoa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC kutokana na masharti mapya iliyotoa dhidi ya wanasaisa kabla ya uchaguzi mkuu ujao.

Nyawa ameitaka Tume hiyo kuzingatia kanuni zake na taratibu za kuandaa uchaguzi na wala sio kila uchao kutoa masharti ambayo yanakinzana na majukumu ya Tume, akisema kuna taasisi zengine za umma zinafaa kuwajibika.

Akizungumza katika mkutano wa kisiasa katika eneo la Mwereni gatuzi dogo la Lungalunga kaunti ya Kwale, Nyawa aliesisitiza haja ya wanasiasa kupewa nafasi ya kuzungumza na wananchi sawa na kueleza sera zao bila ya vizuizi.

Kiongozi huyo wa vijana ambaye alitangaza nia yake ya kuwania kiti cha uwakilishi wadi ya Mwereni wakati wa uchaguzi ujao, amesema taifa la Kenya linazingatia demokrasia na kwamba kila taasisi inafaa kutekeleza majukumu yake.

“Katika uwaja wa siasa IEBC inakuzi moja tu kama msimamizi na kama msimamizi anaanza kutengeza sheria hapo ndipo anakosea, hii Kneya ni nchi ya demokrasia kwa hivyo IEBC isilete sheria nyingi na kufuatilia wanasiasa kuhusu pesa watatumia kwa kampeni, hiyo sio jukumu lake kuna taasisi inaitwa EACC”, alisema Nyawa.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending