News
Waziri Deborah awahimiza wakenya kupanda miti kwa wingi
Serikali imewahimiza wakenya kutumia fursa ya siku ya kitaifa ya mapumzo ya Mazingira Oktoba 10, na kuhakikisha wanajitokeza kwa wingi na kupanda miti ili kudhibiti mabadiliko ya tabia nchi.
Waziri wa Mazingira, mabadiliko ya tabianchi na misitu nchini Deborah Barassa alisema kila mkenya ana jukumu la kutembelea shule za msingi aliyosomea na kutekeleza jukumu lake la kupamba miti.
Deborah alisema hatua hiyo itasaidia pakubwa taifa la Kenya kudhibiti mabadiliko ya tabia nchi sawa na kuafikia azma ya serikali ya kupanda miti bilioni 15 ifikapo mwaka wa 2030.
“Tuko na malengo ya kuhakikisha tunatunza mazingira na hii itafaulu ikiwa tutapanda miti kwa wingi hasa kila mmoja atumie siku ya mazingira na kutembelea shule tumesoma na kupanda miti ili kudhibiti mazingira”, alisema Deborah.
Kwa upande wake Afisa mkuu mtendaji wa Taasisi ya utafiti wa misitu nchini KEFRI Jane Njuguna, amesema maeneo mengi nchini yanakabiliwa na kiangazi kikali kutokana na uhaba wa misitu, akisisitiza haja ya wakenya kutumia siku hiyo kupanda miti.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

