Connect with us

News

Wito wa haki kupatikana watawala mazishi ya Albert Ojwang’

Published

on

Ibada ya mazishi kwa ajili ya mwendazake mwanablogu na mwalimu Albert Ojwang’ aliyeuawa mikononi mwa polisi inafanyika katika shule ya msingi ya Nyawango kaunti ya Homa Bay, huku kukiwa na hali ya taharuki.

Katika hafla hiyo uwepo wa maafisa wa usalama haujashuhudiwa.

Kulingana na Odhiambo Ojiro, mmoja wa wanaharakati katika eneo hilo alisema vijana wamejitolea kumpumzisha Ojwang’ kwa heshima aliyostahili’ na ishara hiyo imeonyesha umoja walionao vijana hao.

Wakizungumza katika hafla hiyo, baadhi ya walimu katika shule ambayo Albert alikuwa akihudumu katika kaunti ya Taita Taveta, wakiongozwa na Ismael Omoke Kongo walishinikiza naibu inspekta jenerali wa Eliud Lagat na wengine waliohusika na mauaji hayo kukamatwa na kufunguliwa mashtaka mahakamani.

Walisema kesi ya mauaji ya dhidi ya Albert inafaa kuchukuliwa kwa uzito na kuharakishwa mahakamani ili haki kwa familia na jamii ipatikane.

“Tunataka hii kesi kuharakishwa na wote waliohusishwa iwe kupitia kutoa maagizo hadi utekelezaji kushtakiwa”, walisema walimu hao

Wanablogu mbali mbali waliofika katika hafla hiyo waliunga mkono kauli ya walimu hao huku wakishikiniza mamlaka ya kutathmini utendakazi wa polisi IPOA na idara ya upelelezi wa makosa ya jinai DCI kuwajibika.

“Yale ambayo mnatenda Mungu anaona, ipo siku sauti zetu zitasikika, mimi naambia IPOA na DCI mnatatiza haki kwa Albert na nataka mmkamate mshtakiwa, na tunaambia serikali huwezi kutuua na utuongoze”, walisema wanablogu.

Ojwang’ alichukuliwa nyumbani kwao kaunti ya Homabay na maafisa wa usalama na kusafirishwa hadi kituo cha polisi cha Central jijini Nairobi ambapo alitangazwa kufariki baadaye.

Wakati huo polisi walitoa taarifa na kudai Albert alifariki baada ya kujigonga kwenye ukuta wa chumba cha seli alimokuwa anazuiliwa kituoni Central.

Mauaji ya Albert yalizua hasira miongoni mwa wakenya hasa vijana wa kizazi cha Gen Z, ambao wamekuwa wakiendeleza misururu ya maandamano nchini.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending