Connect with us

News

Alubbe: Wakaazi wa Pwani hawafahamu haki za ardhi

Published

on

Mkurugenzi mkuu wa shirika la kuangazia haki za ardhi nchini, Kenya Land Alliance KLA, Faith Alubbe amesema kuwa idadi kubwa ya wakaazi hasa wa mashinani wanakumbwa na changamoto za ardhi kufuatia ukosefu wa uelewa na ufahamu wa haki na sheria zinazofungamana na umiliki wa ardhi.

Akizungumza baada ya warsha na wanahabari mjini Malindi kaunti ya Kilifi, Alubbe alikariri kuwa ardhi nyingi za wananchi zinaishia mikononi mwa mabwenyenye kutokana na wakaazi wenyewe hawana namna ya kufahamu au hata kupata elimu kuhusu masuala ya ardhi.

Kufuatia hilo Alubbe alikariri kuwa shirika hilo limeweka mikakati ya kutumia vyombo vya habari kutoa hamasa hizo kwa wananchi hali inayosababisha wao kuandaa warsha za kuwahamasisha wanahabari namna watakavyoweza kupitisha hamasa hizo kuhusu umiliki wa ardhi kwa wananchi kupitia vyombo mbalimbali vya habari.

Warsha na Wanahabari mjini Malindi kaunti ya Kilifi kuhusu ufahamu wa masuala ya ardhi Pwani

“Uskwota umekithiri katika maeneo mengi humu nchini kutokana na suala kuwa hakujakuwa na mifumo hitajika ya kuangazia dhulma za kihistoria za ardhi” alisema Alubbe.

“Ni sharti jamii ipewe taarifa muhimu za jinsi ya kusajili ardhi zao kwani wanajamii wengi wanaishi kwenye ardhi ambazo hawana umiliki nazo kutokana na ukosefu wa ufahamu” aliongeza Alubbe

KLA iliandaa warsha ambayo ilijumuisha wanahabari kutoka kaunti ya Kilifi lakini pia wale wa kaunti ya Tanariver.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending