News
Kindiki: Uchumi wa nchi umeimarika ikilinganishwa na miaka ya nyuma
Naibu wa rais Prof. Kithure Kindiki amesema uchumi wa nchi umeimarika kwa sasa ikilinganishwa na miaka ya nyuma.
Akizungumza katika eneo la Wundanyi kaunti ya Taita Taveta, katika ziara yake ya kuviwezesha vikundi mbalimbali pamoja na vyama vya ushirika wa akiba na mikopo ili kujiendeleza, Prof. Kindiki alisema mikakati ambayo imekuwa ikiwekwa kama ya uimarishaji wa sekta ya kilimo ilichangia kwa hilo kuafikiwa.
Aidha, Prof. Kindiki alisema uchumi wa Kenya ulikuwa umedorora zaidi wakati wa ujio wa uviko 19 ili kwa sasa uko thabiti.
Wakati huohuo, Prof. Kindiki alisema kilimo kimeimarika nchini kupitia ugavi wa mbolea ya bei nafuu ambayo imekuwa ikitolewa na serikali kuu kwa wakulima ili kuwe na utoshelevu wa chakula.

Naibu wa rais Prof. Kithure Kindiki na viongozi wengine katika kaunti ya Taita Taveta.
Vilevile, Prof. Kindiki alisema mpango wa ujenzi wa masoko ya kisasa umeanzishwa na wanapania kujenga masoko kwenye kaunti ya Taita Taveta.
Taarifa ya Janet Mumbi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

