Connect with us

News

Daktari Johansen: Uchunguzi wa miili 34 Kwa Binzaro umebaini watu hao waliuawa

Published

on

Uchunguzi wa miili iliyofukuliwa kutoka kwa makaburi kwenye kijiji cha Kwa Binzaro kaunti ya Kilifi umeonyesha kwamba baadhi ya miili hiyo ni ya watu waliouawa kimakusudi kwa kupigwa na vifaa butu au kunyongwa, jambo ambalo limezua tetesi ya vitu vya lazima.

Kundi la maafisa wa Uchunguzi wa maiti na wataalamu wengine wakiongozwa na mkaguzi mkuu wa maiti wa serikali Daktari Johansen Oduor, kufikia sasa tayari limechunguza miili 34 iliyofukuliwa au kupatikana katika msitu wa kijiji cha Kwa Binzaro.

Maafisa hao waliweka wazi kwamba kuna kila dalili huenda watu hao waliuawa na sio kupitia kufunga hadi kufa kwa mujibu wa imani za kiitikadi.

Uchunguzi huu sasa unzua maswali mengi kuhusu sakata ya Shakahola.

Mapema wiki hii, Watu wanne walifikishwa Mahakamani mjini Malindi wakikabikiwa na kesi ya mauaji ya halaiki ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro.

Hakimu mkuu wa Mahakama ya Malindi Joy Shiundu Wesonga, aliagiza kuendelea kuzuiliwa korokoroni kwa wanne hao kwa siku 60 zaidi hadi kesi yao itakaposikizwa tena mnamo tarehe 2, Oktoba mwaka huu.

Wakati huo huo kitengo cha ufukuzi wa miili tayari kimetambua makaburi zaidi ya wafu yanayoaminika kuzikwa waumini wa dini hiyo potofu.

Washukiwa hao ni pamoja na Kahindi Gharama, Thomas Mukonwe, James Kahindi Kazungu na Sharleen Tembo Anindo wanaohusishwa na mashtaka ya kuendeleza mafunzo ya dini potofu, ugaidi, itikadi kali na uhalifu uliyosababisha baadhi ya waumini kufunga hadi kufariki.

Taarifa ya Eric Ponda

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending