News
LSK yataka mkuu wa kituo cha polisi cha Central-Mombasa kusimamishwa kazi
Chama cha wanasheria nchini (LSK), tawi la Mombasa, kimetaka kusimamishwa kazi mara moja kwa mkuu wa kituo cha polisi cha Central jijini Mombasa pamoja na maafisa wote waliokuwa kazini wakati wa tukio la kifo cha Simon Warui, kilichotokea katika mazingira ya kutatanisha akiwa kizuizini kituoni humo.
Kupitia kwa mwenyekiti wake, wakili Natasha Ali Errey, LSK ilitaja tukio hilo kuwa la kusikitisha na linaloibua maswali mazito kuhusu ukiukaji wa haki za binadamu.
Wakili Natasha alisema kuna dalili za dhuluma au uzembe wa hali ya juu, hivyo ni muhimu kwa maafisa waliokuwa kazini wakati huo kuondolewa kazini kwa muda ili uchunguzi ufanyike bila vikwazo.
Chama hicho pia kilitaka mamlaka huru ya uangalizi wa polisi (IPOA) kuharakisha uchunguzi kuhusu kifo cha Warui, na kuhakikisha kuwa ripoti yake inatolewa hadharani, kwa uwazi na kwa wakati, ili wananchi waweze kufahamu hatua zitakazochukuliwa.
Katika taarifa kwa vyombo vya habari, wakili Natasha alisisitiza kuwa LSK haitalegeza kamba katika kufuatilia suala hilo, na itaendelea kushinikiza haki itendeke kwa familia ya marehemu Warui hadi ukweli utakapofichuka.

Simon Warui anayedaiwa kufariki katika kituo cha polisi cha Central, Mombasa.
Awali taarifa ya polisi katika kituo cha Central jijini Mombasa ilisema Warui alifariki kutokana na majeraha aliyoyapata baada ya kuanguka kutoka kwa ukuta wa seli alipojaribu kuruka.
Hata hivyo ripoti ya upasuaji wa maiti ilibaini kuwa Warui alifariki kutokana na majeraha na ukosefu wa Oksijeni.
Taarifa ya mwanahabari wetu.
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

