News
Mahakama ya Kilifi yamhukumu mwanamme kifungo cha miaka 2 gerezani
Mahakama ya Kilifi imemhukumu kifungo cha miaka miwili gerezani mwanaume mmoja mwenye umri wa miaka 36 kwa kosa la kumpiga bibi yake na kumsababishia majeraha.
Akitoa hukumu hiyo hakimu wa mahakama hiyo Ivy Wasike alisema kuwa mshtakiwa kwa jina Silas Shoka Mupe ana siku 14 kisheria za kukata rufaa iwapo hakuridhishwa na uamuzi huo.
Awali, kabla ya hukumu hiyo mahakama ilielezwa kwamba mnamo tarehe 8 mwezi septemba mwaka 2025, Mupe alimpiga na kumjeruhi bibi yake kwa jina Kadzo Karisa mwenye umri wa miaka 30.

Silas Shoka Mupe aliyehukumiwa kifungo cha miaka 2 gerezani katika mahakama ya Kilifi.
Mahakama hiyo pia ilielezwa kwamba Mupe ambaye ni mume wa bibi wanne na baba wa watoto 12, ana uzoefu wa kuwapiga bibi zake bila sababu za maana na kwamba hajukumiki katika mahitaji ya kimusingi ya watoto wake.
Wakati huo huo, mahakama hio ya Kilifi pia inatarajiwa kutoa uamuzi dhidi ya kesi za wanaume wawili walioshtakiwa kwa makosa ya unajisi: Joseph Kazungu na Elijah Murime.
Hakimu wa mahakama hiyo Ivy Wasike aliwaagiza washtakiwa Kazungu aliyeshtakiwa na kesi ya unajisi wa mtoto mwenye umri wa miaka 11 na Murime aliyeshtakiwa na kesi ya unajisi wa mtoto mwenye umri wa miaka 14, kuzuiliwa rumande hadi tarehe 1 mwezi Oktoba mwaka 2025 ambapo hukumu hiyo itatolewa.
Hakimu huyo aidha aliagiza wadhamini kwenye kesi hizo kurejeshewa udhamini wao, na washukiwa kurejeshwa tena mahakamani mnamo tarehe mosi mwezi Oktoba, 2025 ambapo uamuzi wa kesi hizo utatolewa.
Taarifa ya Teclar Yeri
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

