News
Furaha Chengo ajiuzulu kutoka chama cha DCP
Mgombea wa nafasi ya ubunge wa Magarini kaunti ya Kilifi kwa chama cha Democracy for Citizens Party DCP Furaha Chengo Ngumbao maarufu Kalama Wehu amejiuzulu kutoka chama hicho.
Furaha ambaye ni Wanachama wa Kamati kuu wa kitaifa wa chama hicho, alisema bado yuko kwenye kinyang’anyiro cha ugombea wa ubunge wa Magarini lakini kwa tiketi ya chama kingine.
Katika barau yake kwa makao makuu ya chama hicho, Furaha alitoa sababu za kujiuzulu katika chama hicho ikiwemo ukosefu wa mawasiliano bora, muongozo madhubiti wa chama na kupuuziliwa mbali kwa matakwa ya wakaazi wa Magarini kupitia chama hicho.

Mgombea wa nafasi ya ubunge wa Magarini kaunti ya Kilifi kwa chama cha DCP Furaha Chengo Kalama amejiuzulu kutoka chama hicho.
Hatua hii ni pigo kubwa kwa chama cha DCP katika eneo la Pwani baada ya mgombea mwengine wa eneo bunge la Banisa Adam Mohammed pia kujiuzulu kutoka chama hicho juma lililopita.
Uchaguzi huo mdogo wa Magarini umewavutia, viongozi mbalimbali wakiwemo Harrison Kombe wa ODM, Samuel Nzai wa Wiper, Furaha Chengo Kalama huku Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC imeahidi kuandaa uchaguzi huo Novemba 27 mwaka huu.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

