News
Mboko atoa wito kwa Wakenya kujiepusha na mambo maovu
Mbunge wa Likoni kaunti ya Mombasa Mishi Mboko ametoa wito kwa Wakenya kujiepusha na mambo maovu pamoja na kauli ambazo huenda zikaichafulia jina taifa la Kenya kwani huenda zikaathiri sekta ya utalii.
Mboko ambaye alikuwa akizungumza katika kaunti ya Mombasa, alisema serikali inapaswa kuweka mikakati ifaayo ili kuimarisha sekta ya utalii kupitia uwekezaji.
Aidha, Mboko aliwahimiza Wakenya kudumisha uzalendo na pia kuwa katika mstari wa mbele kujenga taswira nzuri ya taifa la Kenya ili boresha utalii na pia kubuni nafasi za ajira kwa vijana nchini.
“Ni sekta ambayo lazima ipate fedha za kutosha na lazima tuweze kuiboresha sekta hii ili tupunguze ukosefu wa ajira kwa vijana’’ alisema Mboko.
Wakati huo huo, Mboko alisema mila na tamaduni za hapa nchini Kenya zinapaswa kutunzwa kwani ni mojawapo ya vivutio vya utalii.
“Hizi tamaduni zetu ni muhimu sana na lazima tuzidhibiti maana ni njia moja inayotupatia mapato na ni njia moja ya kuvutia mambo ya utalii katika taifa letu’’ aliongeza Mboko.
Taarifa ya Janet Mumbi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

