Connect with us

News

Jeremiah Kioni: Gachagua anafanyakazi kisiri na rais Ruto

Published

on

Katibu Mkuu wa chama cha Jubilee Jeremiah Kioni amedai kuwa aliyekuwa naibu Rais Rigathi Gachagua anafanya kazi na rais William Ruto kisiri.

Kulingana na Kioni, Gachagua alikutana na viongozi katika kaunti ya Narok katika tarehe ambayo haijatajwa, ambapo alijaribu kueleza ni kwa nini chama cha DCP kilikuwa kinamnyima muaniaji wa wadi ya Narok mjini Joshua Ole Kaputa tiketi ya chama hicho kwenye uchaguzi mdogo ujao.

Kioni alidokeza kwamba mkutano huo ulikuwa na wanachama 15, miongoni mwao wakiwemo makasisi na kwamba kulikuwa na mpango uliowekwa kati yake na rais Ruto na Joshua angeteuliwa baadaye.

“Gachagua aliwaambia kuwa William Ruto tayari ametuma wajumbe kwao na walikuwa na mpango wa kuweka vyama vyao katika hali ya udhabiti kisha wakutane kujadiliana,” alidai Kioni.

Kioni hata hivyo alikana kufichua maelezo zaidi kuhusu mkutano huo wa siri, akisema “Alijieleza mwenyewe”.

Alishikilia kuwa chama cha Jubilee kiko tayari kufanya kazi na vyama vyenye nia moja na hakitashirikiana na yeyote anayehusika na mikataba mibaya ya kisiasa.

“Tungependa kufanya kazi na vyama vyenye nia moja ambavyo vinaamini katika kumbandua rais William madarakani “pata watu wako na mimi nipate wangu”, alibainisha Kioni.

Wakati huo huo aliwataka vijana kujiandikisha kuwa wapiga kura kwenye zoezi la usajili endelevu lililoanza rasmi Septemba 29, 2025

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending