Connect with us

News

Gavana Lusaka afutilia mbali baraza lake la mawaziri

Published

on

Gavana wa kaunti ya Bungoma Kenneth Lusaka, amefutilia mbali baraza lake la mawaziri akilenga kulifanyia mabadiliko ili kuimarisha utendakazi wa serikali ya kaunti hiyo.

Katika taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya bahari na kutiwa saini na Gavana huyo, imebaini kwamba Katibu wa kaunti pamoja na Mwanasheria mkuu wa kaunti pia wamesimamishwa kazi, hatua hii ikitekelezwa miezi michache tu kabla ya uchaguzi mkuu ujao mwaka wa 2027.

Katika taarifa hiyo iliyotolewa na serikali ya kaunti hiyo, Gavana Lusaka alieleza kwamba hatua hiyo imetokana na utendakazi duni wa viongozi hao pamoja na kutofikia malengo ya wananchi kwa kuambatana na ajenda za Gavana huyo.

Gavana Lusaka alisema kwa kuzingatia kipengele cha 40 ibara ya kwanza sehemu ya {a}, ambayo inampa mamlaka ya kuwasimamisha kazi maafisa wakuu wa kaunti pamoja na kulivunja baraza la mawaziri, Gavana Lusaka alichukua hatua hiyo ili kuimarisha utendakazi wa kaunti.

Taarifa ya kusimamishwa kazi kwa baraza la mawaziri iliyotolewa na Gavana wa Bungoma Kenneth Lusaka

Taarifa hiyo pia ilifafanua kwamba ilichukuliwa kwa nia njema na kwa maslahi mapana ya umma, ikiongeza kwamba inalenga kuwezesha utendaji bora ndani ya utawala wa kaunti pamoja na kulinda uadilifu wa taasisi za umma.

“Nataka kuwahakikisha wakaazi wa kaunti ya Bungoma kwamba mabadiliko hayo makubwa hayataathiri huduma za kaunti kwani ni hatua moja wapo ya kuboresha utendakazi wa kaunti hiyo”, alisema Gavana.

Aidha alieleza kwamba mawasiliano zaidi kuhusu mipango ya muda na uteuzi mpya yatatolewa baadaye, kwa mujibu wa taratibu za kisheria.

Hata hivyo tetesi kutoka kwa wandani wa kisiasa, walisema kwamba hatua hiyo imechochewa kisiasa ili kuzuia mchakato uliyokuwa umepangwa wa kuwasilisha hoja bungeni ya kuwabandua uongozi baadhi ya mawaziri wa serikali ya kaunti hiyo kutokana na utendakazi duni na ufisadi.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending