News
Gharama ya matibabu na uhaba wa dawa umeathiri juhudi za kudhibiti ugonjwa wa figo
Ulimwengu umeadhimisha siku ya kimatiafa ya Figo dunianihuku ikibainika kuwa gharama kubwa za matibabu pamoja na uhaba wa dawa katika hospitali za umma nchini ni miongoni mwa changamoto kuu zinazokwamisha juhudi za kukabiliana na ugonjwa wa figo.
Wagonjwa wa figo waliopata matibabu na wanaoendelea kutumia dawa walisema hali hiyo imefanya matibabu kuwa mzigo mkubwa kwao na familia zao.
Wakizungumza wakati wa maadhimisho ya siku ya Figo duniani yaliyofanyika katika uwanja wa Karisa Maitha mjini Kilifi, kaunti ya Kilifi, wagonjwa hao waliitaka serikali kuingilia kati ili kupunguza gharama za matibabu na kuhakikisha dawa zinapatikana kwa urahisi katika hospitali za umma.
Aidha, wagonjwa hao walilalamikia ukosefu wa taasisi za kupandikiza figo nchini wakisema hali hiyo inalazimu baadhi yao kusafiri hadi mataifa ya nje ili kupata huduma hiyo, jambo linaloongeza gharama na kuchelewesha matibabu.
Kwa upande wao, wauguzi wa ugonjwa wa figo wakiongozwa na Daniel Masha pamoja na Fatuma Bashir walikiri kuwepo kwa changamoto hizo huku wakisema kuna haja ya serikali kubuni mikakati madhubuti ya kuhakikisha gharama za matibabu ya figo zinadhibitiwa kikamilifu kupitia mpango wa Bima ya Afya ya Jamii (SHA).
Masha pia alipendekeza kuanzishwa kwa taasisi maalum za kupandikiza figo katika kila kaunti, pamoja na kuajiri wataalamu wa kutosha ili kuboresha huduma kwa wagonjwa wa figo nchini.
Naye mtaalamu wa afya ya figo, Daktari Andrew, alisisitiza umuhimu wa kuongeza hamasa kwa umma kuhusu ugonjwa wa figo. Amesema uhamasishaji utasaidia wananchi kutambua dalili mapema na kuchukua hatua za matibabu kwa wakati.
Daktari Andrew pia aliwahimiza wananchi kujenga utamaduni wa kufanyiwa uchunguzi wa afya mara kwa mara, akipendekeza kila mtu kutembelea kituo cha afya angalau mara moja kwa mwaka kwa ajili ya uchunguzi wa jumla wa afya.
Maadhimisho ya siku ya Figo duniani hufanyika kila mwaka kwa lengo la kuongeza uelewa kuhusu magonjwa ya figo, umuhimu wa kinga, na upatikanaji wa matibabu kwa wagonjwa duniani kote.
Taarifa ya Elizabeth Mwende
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

